< Mithali 20 >
1 Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
En Spotter er Vinen, stærk Drik slaar sig løs, og ingen, som raver deraf, er viis.
2 Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
Som Løvebrøl er Rædslen, en Konge vækker, at vække hans Vrede er at vove sit Liv.
3 Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
Mands Ære er det at undgaa Trætte, men alle Taaber vil Strid.
4 Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
Om Efteraaret pløjer den lade ikke, han søger i Høst, men finder intet.
5 Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
Raad i Mands Hjerte er dybe Vande, men Mand med Indsigt drager det op.
6 Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
Mangen kaldes en velvillig Mand, men hvem kan finde en trofast Mand?
7 Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
Retfærdig er den, som lydefrit vandrer, hans Sønner faar Lykke efter ham.
8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
Kongen, der sidder i Dommersædet, sigter alt ondt med sit Blik.
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
Hvo kan sige: »Jeg rensed mit Hjerte, og jeg er ren for Synd!«
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
To Slags Vægt og to Slags Maal, begge Dele er HERREN en Gru.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
Selv Drengen kendes paa det, han gør, om han er ren og ret hans Færd.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
Øret, der hører, og Øjet, der ser, HERREN skabte dem begge.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
Elsk ikke Søvn, at du ej bliver fattig, luk Øjnene op og bliv mæt.
14 “Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
Køberen siger: »Usselt, usselt!« men skryder af Handelen, naar han gaar bort.
15 Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
Har man end Guld og Perler i Mængde, kosteligst Smykke er Kundskabslæber.
16 Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
Tag hans Klæder, han borged for en anden, pant ham for fremmedes Skyld!
17 Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
Sødt smager Løgnens Brød, bagefter fyldes Munden med Grus.
18 Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
Planer, der lægges ved Raadslagning, lykkes; før Krig efter modent Overlæg!
19 Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
Bagtaleren røber, hvad ham er betroet, hav ej med en aabenmundet at gøre!
20 Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
Den, der bander Fader og Moder, i Bælgmørke gaar hans Lampe ud.
21 Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
Først haster man efter en Arv, men til sidst velsignes den ikke.
22 Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
Sig ikke: »Ondt vil jeg gengælde!« Bi paa HERREN, saa hjælper han dig.
23 Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
To Slags Lodder er HERREN en Gru, det er ikke godt, at Vægten er falsk.
24 Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
Fra HERREN er Mands Fjed, hvor kan et Menneske fatte sin Skæbne!
25 Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
Det er farligt at sige tankeløst: »Helligt!« og først efter Løftet tænke sig om.
26 Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
Viis Konge sigter de gudløse, lader Tærskehjul gaa over dem.
27 Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
Menneskets Aand er en HERRENS Lampe, den ransager alle hans Indres Kamre.
28 Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
Godhed og Troskab vogter Kongen, han støtter sin Trone ved Retfærd.
29 Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
Unges Stolthed er deres Styrke, gamles Smykke er graanet Haar.
30 Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.
Blodige Strimer renser den onde og Hug hans Indres Kamre.