< Mithali 20 >

1 Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
Víno činí posměvače, a nápoj opojný nepokojného; pročež každý, kdož se kochá v něm, nebývá moudrý.
2 Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
Hrůza královská jako řvání mladého lva; kdož ho rozhněvá, hřeší proti životu svému.
3 Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
Přestati od sváru jest to každému ku poctivosti, ale kdožkoli se do nich zapletá, blázen jest.
4 Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
Lenoch neoře pro zimu, pročež žebrati bude ve žni, ale nadarmo.
5 Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
Rada v srdci muže voda hluboká, muž však rozumný dosáhne jí.
6 Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
Větší díl lidí honosí se účinností svou, ale v pravdě takového kdo nalezne?
7 Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
Spravedlivý ustavičně chodí v upřímnosti své; blažení synové jeho po něm.
8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
Král sedě na soudné stolici, rozhání očima svýma všecko zlé.
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
Kdo může říci: Očistil jsem srdce své? Èist jsem od hříchu svého?
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
Závaží rozdílná a míra rozdílná, obé to ohavností jest Hospodinu.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
Po skutcích svých poznáno bývá také i pachole, jest-li upřímé a pravé dílo jeho.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
Ucho, kteréž slyší, a oko, kteréž vidí, obé to učinil Hospodin.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
Nemiluj snu, abys nezchudl, otevři oči své, a nasytíš se chlebem.
14 “Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
Zlé, zlé, říká ten, kdož kupuje, a odejda, tedy se chlubí.
15 Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
Zlato a množství perel, a nejdražší klínot jsou rtové umělí.
16 Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
Vezmi roucho toho, kterýž slíbil za cizího, a kdo za cizozemku, základ jeho.
17 Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
Chutný jest někomu chléb falše, ale potom ústa jeho pískem naplněna bývají.
18 Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
Myšlení radou upevňuj, a s opatrnou radou veď boj.
19 Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
Kdo vynáší tajnost, chodí neupřímě, pročež k lahodícímu rty svými nepřiměšuj se.
20 Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
Kdo zlořečí otci svému neb matce své, zhasne svíce jeho v temných mrákotách.
21 Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
Dědictví rychle z počátku nabytému naposledy nebývá dobrořečeno,
22 Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
Neříkej: Odplatím se zlým; očekávej na Hospodina, a vysvobodí tě.
23 Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
Ohavností jsou Hospodinu závaží rozdílná, a váhy falešné neoblibuje.
24 Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
Od Hospodina jsou krokové muže, ale člověk jak vyrozumívá cestě jeho?
25 Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
Osídlo jest člověku pohltiti věc posvěcenou, a po slibu zase toho vyhledávati.
26 Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
Král moudrý rozptyluje bezbožné, a uvodí na ně pomstu.
27 Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
Duše člověka jest svíce Hospodinova, kteráž zpytuje všecky vnitřnosti srdečné.
28 Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
Milosrdenství a pravda ostříhají krále, a milosrdenstvím podpírá se trůn jeho.
29 Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
Ozdoba mládenců jest síla jejich, a okrasa starců šediny.
30 Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.
Modřiny ran jsou lékařství při zlém, a bití vnitřnostem života.

< Mithali 20 >