< Mithali 2 >
1 Mwanangu, kama ukiyapokea maneno yangu na kuzitunza amri zangu,
我儿,你若领受我的言语, 存记我的命令,
2 usikilize hekima na utaelekeza moyo wako katika ufahamu.
侧耳听智慧, 专心求聪明,
3 kama utalilia ufahamu na kupaza sauti yako kwa ajili ya ufahamu,
呼求明哲, 扬声求聪明,
4 kama utautafuta kama fedha na kupekua ufahamu kama unatafuta hazina iliyojificha,
寻找它,如寻找银子, 搜求它,如搜求隐藏的珍宝,
5 ndipo utakapofahamu hofu ya Yehova na utapata maarifa ya Mungu.
你就明白敬畏耶和华, 得以认识 神。
6 Kwa kuwa Yohova hutoa hekima, katika kinywa chake hutoka maarifa na ufahamu.
因为,耶和华赐人智慧; 知识和聪明都由他口而出。
7 Yeye huhifadhi sauti ya hekima kwa wale wampendezao, yeye ni ngao kwa wale waendao katika uadilifu,
他给正直人存留真智慧, 给行为纯正的人作盾牌,
8 huongoza katika njia za haki na atalinda njia ya waaminifu kwake.
为要保守公平人的路, 护庇虔敬人的道。
9 Ndipo utakapoelewa wema, haki, usawa na kila njia njema.
你也必明白仁义、公平、 正直、一切的善道。
10 Maana hekima itaingia moyoni mwako na maarifa yataipendeza nafsi yako.
智慧必入你心; 你的灵要以知识为美。
11 Busara itakulinda, ufahamu utakuongoza.
谋略必护卫你; 聪明必保守你,
12 Vitakuokoa kutoka katika njia ya uovu, kutoka kwa wale waongeao mambo potovu.
要救你脱离恶道, 脱离说乖谬话的人。
13 Ambao huziacha njia za wema na kutembea katika njia za giza.
那等人舍弃正直的路, 行走黑暗的道,
14 Hufurahia wanapotenda maovu na hupendezwa katika upotovu.
欢喜作恶, 喜爱恶人的乖僻,
15 Hufuata njia za udanganyifu na kwa kutumia ghilba huficha mapito yao.
在他们的道中弯曲, 在他们的路上偏僻。
16 Busara na hekima zitakuokoa kutoka kwa mwanamke malaya, kutoka kwa mwanamke anayetafuta visa na mwenye maneno ya kubembeleza.
智慧要救你脱离淫妇, 就是那油嘴滑舌的外女。
17 Yeye humwacha mwenzi wa ujana wake na kusahau agano la Mungu wake.
她离弃幼年的配偶, 忘了 神的盟约。
18 Maana nyumba yake huinama na kufa na mapito yake yatakupeleka kwa wale walioko kaburini.
她的家陷入死地; 她的路偏向阴间。 ()
19 Wote waiendeao njia yake hawatarudi tena na wala hawataziona njia za uzima.
凡到她那里去的,不得转回, 也得不着生命的路。
20 kwa hiyo utatembea katika njia ya watu wema na kufuata njia za wale watendao mema.
智慧必使你行善人的道, 守义人的路。
21 Kwa wale watendao mema watafanya makazi yao katika nchi, na wale wenye uadilifu watadumu katika nchi.
正直人必在世上居住; 完全人必在地上存留。
22 Lakini waovu wataondolewa katika nchi na wale wasioamini wataondolewa katika nchi.
惟有恶人必然剪除; 奸诈的,必然拔出。