< Mithali 19 >

1 Bora mtu masikini ambaye huenenda katika uadilifu wake kuliko mwenye ukaidi katika maneno yake na ni mpumbavu.
Mejor es ser pobre y honesto, que un tonto y mentiroso.
2 Tena, si vizuri kuwa na hamu bila maarifa na mwenye kukimbia haraka sana hukosea njia.
No es bueno ser de los que no piensan. Si actúas con afán, cometerás errores.
3 Upuuzi wa mtu unaharibu maisha yake na moyo wake hughadhabika dhidi ya Yehova.
La gente destruye su vida por causa de su propia estupidez, y se enojan con el Señor.
4 Utajiri huongeza marafiki wengi, bali mtu masikini hutengwa na rafiki zake.
Si eres rico, tendrás muchos amigos; pero si eres pobre, perderás todos los amigos que tenías.
5 Shahidi wa uongo hatakosa adhabu na mwenye kupumua uongo hataokoka.
El testigo falso será castigado; los mentirosos no podrán escaparse con sus mentiras.
6 Wengi wataomba fadhila kutoka kwa mtu mkarimu na kila mtu ni rafiki wa yule anayetoa zawadi.
Muchos piden favores a personas importantes, y todos son amigos del que es generoso.
7 Mtu masikini huchukiwa na ndugu zake wote; je marafiki wengi kiasi gani hujitenga kutoka kwake! Anawaita, lakini wameondoka.
Si los familiares del pobre no lo pueden soportar, ¡cuanto menos lo evitarán sus amigos! El tratará de hablarles, pero ellos no lo escucharán.
8 Anayepata hekima huyapenda maisha yake mwenyewe; yeye atunzaye ufahamu atapata kilicho chema.
Si te vuelves sabio, tendrás amor propio; si aprendes a tener buen juicio, serás exitoso.
9 Shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa, bali mwenye kupumua uongo ataangamia.
El testigo falso será castigado, y los mentirosos perecerán.
10 Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa- wala kwa mtumwa kutawala juu ya wafalme.
No es correcto que los tontos vivan en medio de lujos, e incluso es peor que un esclavo gobierne por encima de los líderes.
11 Busara humfanya mtu achelewe kukasirika na utukufu wake ni kusamehe kosa.
Si tienes inteligencia, serás lento para enojarte. Serás respetado al perdonar ofensas.
12 Ghadhabu ya mfalme ni kama muungurumo wa simba kijana, bali fadhila yake ni kama umande kwenye majani.
Cuando un rey se enoja, se escucha como un león rugiente. Pero su bondad es tan suave como el rocío sobre la hierba.
13 Mwana mpumbavu ni uharibifu kwa baba yake na mke mgomvi ni maji yanayochuruzika daima.
Un hijo tonto trae miseria a su padre, y una esposa conflictiva es como una gotera que nunca se seca.
14 Nyumba na utajiri ni urithi kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.
De tu padre heredarás una casa y riquezas; pero una esposa prudente es un regalo de Dios.
15 Uvivu unamtupa mtu kwenye usingizi mzito, bali asiyetamani kufanya kazi atakwenda njaa.
Los perezosos se quedan dormidos con frecuencia; pero su holgazanería indica que están hambrientos.
16 Yeye anayetii amri huyaongoza maisha yake, bali mtu asiyefikiri juu ya njia zake atakufa.
Guarda los mandamientos y vivirás. Recházalos y morirás.
17 Mwenye ukarimu kwa masikini humkopesha Yehova na atalipwa kwa kile alichofanya.
Si eres bondadoso con el pobre, estarás prestándole al Señor, y él te pagará con creces por lo que has hecho.
18 Mrudi mwanao wakati kuna matumaini na usiwe na shauku ya kumweka katika mauti.
Disciplina a tu hijo cuando aún hay tiempo, pero no lo mates.
19 Mtu mwenye hasira kali lazima alipe adhabu; kama ukimwokoa, utafanya hivyo mara mbili.
Los que se enojan con facilidad tienen que pagar el precio por ello. Si les ayudas, tendrás que hacerlo de nuevo.
20 Sikiliza ushauri na ukubali maelekezo, ili uweze kuwa na hekima mwishoni mwa maisha yako.
Escucha el consejo y acepta la instrucción, para que con el tiempo te vuelvas sabio.
21 Moyoni mwa mtu kuna mipango mingi, bali kusudi la Yehova ndilo litakalo simama.
Los seres humanos hacen planes en sus mentes, pero la decisión final es del Señor.
22 Shauku ya mtu ni uaminifu na mtu masikini ni bora kuliko muongo.
El deseo más profundo de todas las personas es el amor sincero. Mejor es ser pobre que un mentiroso.
23 Kumheshimu Yehova huwaelekeza watu kwenye uzima; mwenye nayo atashibishwa na hatadhurika kwa madhara.
Honrar al Señor es vida, y podrás descansar confiado, libre de todo mal.
24 Mtu goigoi huuzika mkono wake ndani ya dishi; hataurudisha juu ya kinywa chake.
Los perezosos llevan su mano al plato, y ni siquiera la levantan para poner la comida en su boca.
25 Kama utampiga mwenye mzaha, wajinga watakuwa na hekima; mwelekeze mwenye ufahamu, naye atapata maarifa.
Si castigas al burlador, puede que estés instruyendo a un inmaduro. Corrige al sabio, y será más sabio.
26 Anayempora baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana anayeleta aibu na shutuma.
Un hijo que abusa de su padre y ahuyenta a su madre, acarrea vergüenza y desgracia.
27 Mwanangu, kama utaacha kusikiliza maelekezo, utapotea kutoka kwenye maneno ya maarifa.
Hijo mío, cuando dejes de escuchar mi instrucción pronto dejarás de seguir la sabiduría.
28 Shahidi mpotofu huidhihaki haki na kinywa cha waovu humeza uovu.
El testigo deshonesto se burla de la justicia, y el malvado se sacia de maldad.
29 Hukumu ipo tayari kwa wenye dhihaka na mjeledi kwa migongo ya wapumbavu.
El castigo está preparado para los burladores, y el azote para las espaldas de los tontos.

< Mithali 19 >