< Mithali 19 >

1 Bora mtu masikini ambaye huenenda katika uadilifu wake kuliko mwenye ukaidi katika maneno yake na ni mpumbavu.
Better is a poor [man] that walketh in his integrity, than he that is perverse in his lips, and is a fool.
2 Tena, si vizuri kuwa na hamu bila maarifa na mwenye kukimbia haraka sana hukosea njia.
Also that a person be without knowledge is not good; and he that hasteth with his feet maketh false steps.
3 Upuuzi wa mtu unaharibu maisha yake na moyo wake hughadhabika dhidi ya Yehova.
The folly of man distorteth his way, and his heart is irritated against Jehovah.
4 Utajiri huongeza marafiki wengi, bali mtu masikini hutengwa na rafiki zake.
Wealth addeth many friends; but the poor is separated from his friend.
5 Shahidi wa uongo hatakosa adhabu na mwenye kupumua uongo hataokoka.
A false witness shall not be held innocent, and he that uttereth lies shall not escape.
6 Wengi wataomba fadhila kutoka kwa mtu mkarimu na kila mtu ni rafiki wa yule anayetoa zawadi.
Many court the favour of a noble; and every one is friend to a man that giveth.
7 Mtu masikini huchukiwa na ndugu zake wote; je marafiki wengi kiasi gani hujitenga kutoka kwake! Anawaita, lakini wameondoka.
All the brethren of a poor [man] hate him; how much more do his friends go far from him: he pursueth [them] with words, — they are not [to be found].
8 Anayepata hekima huyapenda maisha yake mwenyewe; yeye atunzaye ufahamu atapata kilicho chema.
He that getteth sense loveth his own soul; he that keepeth understanding shall find good.
9 Shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa, bali mwenye kupumua uongo ataangamia.
A false witness shall not be held innocent, and he that uttereth lies shall perish.
10 Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa- wala kwa mtumwa kutawala juu ya wafalme.
Good living beseemeth not a fool; how much less for a servant to have rule over princes.
11 Busara humfanya mtu achelewe kukasirika na utukufu wake ni kusamehe kosa.
The discretion of a man maketh him slow to anger, and it is his glory to pass over a transgression.
12 Ghadhabu ya mfalme ni kama muungurumo wa simba kijana, bali fadhila yake ni kama umande kwenye majani.
The king's displeasure is as the roaring of a lion; but his favour is as dew upon the grass.
13 Mwana mpumbavu ni uharibifu kwa baba yake na mke mgomvi ni maji yanayochuruzika daima.
A foolish son is the calamity of his father; and the contentions of a wife are a continual dropping.
14 Nyumba na utajiri ni urithi kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.
House and wealth are an inheritance from fathers; but a prudent wife is from Jehovah.
15 Uvivu unamtupa mtu kwenye usingizi mzito, bali asiyetamani kufanya kazi atakwenda njaa.
Slothfulness casteth into a deep sleep, and the idle soul shall suffer hunger.
16 Yeye anayetii amri huyaongoza maisha yake, bali mtu asiyefikiri juu ya njia zake atakufa.
He that keepeth the commandment keepeth his soul; he that is careless of his ways shall die.
17 Mwenye ukarimu kwa masikini humkopesha Yehova na atalipwa kwa kile alichofanya.
He that is gracious to the poor lendeth unto Jehovah; and what he hath bestowed will he repay unto him.
18 Mrudi mwanao wakati kuna matumaini na usiwe na shauku ya kumweka katika mauti.
Chasten thy son, seeing there is hope; but set not thy soul upon killing him.
19 Mtu mwenye hasira kali lazima alipe adhabu; kama ukimwokoa, utafanya hivyo mara mbili.
A man of great wrath shall suffer punishment; for if thou deliver [him], yet thou must do it again.
20 Sikiliza ushauri na ukubali maelekezo, ili uweze kuwa na hekima mwishoni mwa maisha yako.
Hear counsel, and receive instruction, that thou mayest be wise in thy latter end.
21 Moyoni mwa mtu kuna mipango mingi, bali kusudi la Yehova ndilo litakalo simama.
Many are the thoughts in a man's heart, but the counsel of Jehovah, that doth stand.
22 Shauku ya mtu ni uaminifu na mtu masikini ni bora kuliko muongo.
The charm of a man is his kindness; and a poor [man] is better than a liar.
23 Kumheshimu Yehova huwaelekeza watu kwenye uzima; mwenye nayo atashibishwa na hatadhurika kwa madhara.
The fear of Jehovah [tendeth] to life, and he [that hath it] shall rest satisfied without being visited with evil.
24 Mtu goigoi huuzika mkono wake ndani ya dishi; hataurudisha juu ya kinywa chake.
A sluggard burieth his hand in the dish, and will not even bring it to his mouth again.
25 Kama utampiga mwenye mzaha, wajinga watakuwa na hekima; mwelekeze mwenye ufahamu, naye atapata maarifa.
Smite a scorner, and the simple will beware; reprove the intelligent, and he will understand knowledge.
26 Anayempora baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana anayeleta aibu na shutuma.
He that ruineth [his] father and chaseth away [his] mother is a son that causeth shame and bringeth reproach.
27 Mwanangu, kama utaacha kusikiliza maelekezo, utapotea kutoka kwenye maneno ya maarifa.
Cease, my son, to hear the instruction which causeth to stray from the words of knowledge.
28 Shahidi mpotofu huidhihaki haki na kinywa cha waovu humeza uovu.
A witness of Belial scorneth judgment, and the mouth of the wicked swalloweth down iniquity.
29 Hukumu ipo tayari kwa wenye dhihaka na mjeledi kwa migongo ya wapumbavu.
Judgments are prepared for scorners, and stripes for the back of the foolish.

< Mithali 19 >