< Mithali 18 >

1 Yule ambaye hujitenga hutafuta matakwa yake mwenyewe na hupingana na hukumu zote za kweli.
Los egoístas solo se complacen a sí mismos. Atacan todo lo que procede de la inteligencia.
2 Mpumbavu hapati raha katika ufahamu, lakini hufunua kile kilichopo katika moyo wake.
A los necios no les importa entender, sino solo expresar sus opiniones.
3 Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pamoja naye- sambamba na aibu na shutuma.
Con la maldad viene el desprecio, y con la deshonra viene la desgracia.
4 Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina kirefu; chemchemi ya hekima ni mkondo unaotiririka.
Las palabras de las personas pueden ser profundas como las aguas; como una corriente que brota y es la fuente de la sabiduría.
5 Si vema kuwa na upendeleo kwa mwovu, wala haifai kukana haki kwa wale watendao mema.
No es correcto mostrar preferencia con el culpable y privar al inocente de la justicia.
6 Midomo ya mpumbavu huletea mafarakano na kinywa chake hukaribisha mapigo.
Las palabras de los necios los meten en problemas, como si pidieran a gritos una paliza.
7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na hujinasa mwenye kwa midomo yake.
Los necios caen por sus propias palabras. Sus propias palabras los enredan en una trampa.
8 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu na hushuka katika sehema za ndani sana kwenye mwili.
Escuchar chismes es como comer bocados de tu comida favorita. Llegan hasta lo más profundo.
9 Basi, ambaye ni mzembe katika kazi yake ni ndugu yake anayeharibu wengi.
La pereza y la destrucción son hermanos.
10 Jina la Yehova ni mnara imara; atendaye haki hukimbilia na kuwa salama.
El Señor es una torre protectora para los justos, bajo la cual pueden estar seguros.
11 Mali ya tajiri ni mji wake imara na katika fikira zake ni kama ukuta mrefu.
Los ricos ven la riqueza como una ciudad fortificada. Es como un muro alto en su imaginación.
12 Moyo wa mtu huwa na kiburi kabla ya anguko lake, bali unyenyekevu hutangulia kabla ya heshima.
El orgullo conduce a la destrucción. La humildad precede a la honra.
13 Anayejibu kabla ya kusikiliza- ni upuuzi na aibu yake.
Responder antes de escuchar es estupidez y vergüenza.
14 Roho ya mtu itajinusuru na madhara, bali roho iliyopondeka nani anaweza kuivumilia?
Con un espíritu valiente podrás combatir la enfermedad, pero si tu espíritu está quebrantado, será imposible soportarla.
15 Moyo wa mwenye akili hujipatia maarifa na usikivu wa mwenye busara huitafuta.
Una mente inteligente adquiere conocimiento; los sabios están prestos para escuchar el conocimiento.
16 Zawadi ya mtu inaweza kufungua njia na kumleta mbele ya mtu muhimu.
Un don abrirá puertas para ti, y te llevará a la presencia de personas importantes.
17 Wa kwanza kujitetea katika shitaka lake huonekana kuwa na haki hadi mpinzani wake aje na kumuuliza maswali.
La primera persona en alegar un caso estará en lo correcto hasta que alguien llegue a examinarlos.
18 Kupiga kura kunamaliza mabishano na kuwatawanya wapinzani imara.
Entre los poderosos echar suertes puede acabar una disputa y mostrar la decisión correcta.
19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kushawishiwa kuliko mji wenye nguvu, na kugombana ni kama makomeo ya ngome.
Un hermano a quien has ofendido será más difícil de reconquistar que una ciudad fortificada. Las peleas separan a las personas como barras en las puertas de un castillo.
20 Tumbo la mtu litashiba kutoka kwenye tunda la kinywa chake; atatoshelezwa kwa mavuno ya midomo yake.
Asegúrate de estar en paz con lo que dices, porque siempre tendrás que vivir con tus palabras.
21 Uzima na kifo hutawaliwa kwa ulimi, na wale wenye kuupenda ulimi watakula tunda lake.
Tus palabras tienen el poder de traer vida o muerte; aquellos que disfrutan hablar mucho tendrán que vivir con las consecuencias.
22 Yeye apataye mke anapata kitu chema na kupokea fadhila kutoka kwa Yehova.
Si encuentras una esposa has hallado un bien, y serás bendecido por el Señor.
23 Mtu masikini huomba rehema, lakini mtu tajiri hujibu kwa ukali.
Los pobres ruegan por misericordia, pero los ricos responden con dureza.
24 Anayejidai kwa marafiki wengi watamleta katika uharibifu, bali yupo rafiki ambaye huwa karibu kuliko ndugu.
Algunos amigos te abandonarán, pero hay un amigo que estará más cercano que un hermano.

< Mithali 18 >