< Mithali 18 >
1 Yule ambaye hujitenga hutafuta matakwa yake mwenyewe na hupingana na hukumu zote za kweli.
Celui qui se tient à l’écart cherche ce qui lui plaît, Il s’irrite contre tout ce qui est sage.
2 Mpumbavu hapati raha katika ufahamu, lakini hufunua kile kilichopo katika moyo wake.
Ce n’est pas à l’intelligence que l’insensé prend plaisir, C’est à la manifestation de ses pensées.
3 Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pamoja naye- sambamba na aibu na shutuma.
Quand vient le méchant, vient aussi le mépris; Et avec la honte, vient l’opprobre.
4 Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina kirefu; chemchemi ya hekima ni mkondo unaotiririka.
Les paroles de la bouche d’un homme sont des eaux profondes; La source de la sagesse est un torrent qui jaillit.
5 Si vema kuwa na upendeleo kwa mwovu, wala haifai kukana haki kwa wale watendao mema.
Il n’est pas bon d’avoir égard à la personne du méchant, Pour faire tort au juste dans le jugement.
6 Midomo ya mpumbavu huletea mafarakano na kinywa chake hukaribisha mapigo.
Les lèvres de l’insensé se mêlent aux querelles, Et sa bouche provoque les coups.
7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na hujinasa mwenye kwa midomo yake.
La bouche de l’insensé cause sa ruine, Et ses lèvres sont un piège pour son âme.
8 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu na hushuka katika sehema za ndani sana kwenye mwili.
Les paroles du rapporteur sont comme des friandises, Elles descendent jusqu’au fond des entrailles.
9 Basi, ambaye ni mzembe katika kazi yake ni ndugu yake anayeharibu wengi.
Celui qui se relâche dans son travail Est frère de celui qui détruit.
10 Jina la Yehova ni mnara imara; atendaye haki hukimbilia na kuwa salama.
Le nom de l’Éternel est une tour forte; Le juste s’y réfugie, et se trouve en sûreté.
11 Mali ya tajiri ni mji wake imara na katika fikira zake ni kama ukuta mrefu.
La fortune est pour le riche une ville forte; Dans son imagination, c’est une haute muraille.
12 Moyo wa mtu huwa na kiburi kabla ya anguko lake, bali unyenyekevu hutangulia kabla ya heshima.
Avant la ruine, le cœur de l’homme s’élève; Mais l’humilité précède la gloire.
13 Anayejibu kabla ya kusikiliza- ni upuuzi na aibu yake.
Celui qui répond avant d’avoir écouté Fait un acte de folie et s’attire la confusion.
14 Roho ya mtu itajinusuru na madhara, bali roho iliyopondeka nani anaweza kuivumilia?
L’esprit de l’homme le soutient dans la maladie; Mais l’esprit abattu, qui le relèvera?
15 Moyo wa mwenye akili hujipatia maarifa na usikivu wa mwenye busara huitafuta.
Un cœur intelligent acquiert la science, Et l’oreille des sages cherche la science.
16 Zawadi ya mtu inaweza kufungua njia na kumleta mbele ya mtu muhimu.
Les présents d’un homme lui élargissent la voie, Et lui donnent accès auprès des grands.
17 Wa kwanza kujitetea katika shitaka lake huonekana kuwa na haki hadi mpinzani wake aje na kumuuliza maswali.
Le premier qui parle dans sa cause paraît juste; Vient sa partie adverse, et on l’examine.
18 Kupiga kura kunamaliza mabishano na kuwatawanya wapinzani imara.
Le sort fait cesser les contestations, Et décide entre les puissants.
19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kushawishiwa kuliko mji wenye nguvu, na kugombana ni kama makomeo ya ngome.
Des frères sont plus intraitables qu’une ville forte, Et leurs querelles sont comme les verrous d’un palais.
20 Tumbo la mtu litashiba kutoka kwenye tunda la kinywa chake; atatoshelezwa kwa mavuno ya midomo yake.
C’est du fruit de sa bouche que l’homme rassasie son corps, C’est du produit de ses lèvres qu’il se rassasie.
21 Uzima na kifo hutawaliwa kwa ulimi, na wale wenye kuupenda ulimi watakula tunda lake.
La mort et la vie sont au pouvoir de la langue; Quiconque l’aime en mangera les fruits.
22 Yeye apataye mke anapata kitu chema na kupokea fadhila kutoka kwa Yehova.
Celui qui trouve une femme trouve le bonheur; C’est une grâce qu’il obtient de l’Éternel.
23 Mtu masikini huomba rehema, lakini mtu tajiri hujibu kwa ukali.
Le pauvre parle en suppliant, Et le riche répond avec dureté.
24 Anayejidai kwa marafiki wengi watamleta katika uharibifu, bali yupo rafiki ambaye huwa karibu kuliko ndugu.
Celui qui a beaucoup d’amis les a pour son malheur, Mais il est tel ami plus attaché qu’un frère.