< Mithali 18 >
1 Yule ambaye hujitenga hutafuta matakwa yake mwenyewe na hupingana na hukumu zote za kweli.
Celui qui se tient à l’écart recherche ce qui lui plaît; il conteste contre toute sagesse.
2 Mpumbavu hapati raha katika ufahamu, lakini hufunua kile kilichopo katika moyo wake.
Le sot ne prend pas plaisir à l’intelligence, mais à ce que son cœur soit manifesté.
3 Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pamoja naye- sambamba na aibu na shutuma.
Quand vient le méchant, le mépris vient aussi, et avec l’ignominie, l’opprobre.
4 Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina kirefu; chemchemi ya hekima ni mkondo unaotiririka.
Les paroles de la bouche d’un homme sont des eaux profondes, et la fontaine de la sagesse est un torrent qui coule.
5 Si vema kuwa na upendeleo kwa mwovu, wala haifai kukana haki kwa wale watendao mema.
Ce n’est pas bien d’avoir acception de la personne du méchant pour faire frustrer le juste dans le jugement.
6 Midomo ya mpumbavu huletea mafarakano na kinywa chake hukaribisha mapigo.
Les lèvres du sot entrent en dispute, et sa bouche appelle les coups.
7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake na hujinasa mwenye kwa midomo yake.
La bouche du sot est sa ruine, et ses lèvres sont un piège pour son âme.
8 Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu na hushuka katika sehema za ndani sana kwenye mwili.
Les paroles du rapporteur sont comme des friandises, et elles descendent jusqu’au-dedans des entrailles.
9 Basi, ambaye ni mzembe katika kazi yake ni ndugu yake anayeharibu wengi.
Celui-là aussi qui est lâche dans son ouvrage est frère du destructeur.
10 Jina la Yehova ni mnara imara; atendaye haki hukimbilia na kuwa salama.
Le nom de l’Éternel est une forte tour; le juste y court et s’y trouve en une haute retraite.
11 Mali ya tajiri ni mji wake imara na katika fikira zake ni kama ukuta mrefu.
Les biens du riche sont sa ville forte, et comme une haute muraille, dans son imagination.
12 Moyo wa mtu huwa na kiburi kabla ya anguko lake, bali unyenyekevu hutangulia kabla ya heshima.
Avant la ruine le cœur de l’homme s’élève, et la débonnaireté va devant la gloire.
13 Anayejibu kabla ya kusikiliza- ni upuuzi na aibu yake.
Répondre avant d’avoir entendu, c’est une folie et une confusion pour qui le fait.
14 Roho ya mtu itajinusuru na madhara, bali roho iliyopondeka nani anaweza kuivumilia?
L’esprit d’un homme soutient son infirmité; mais l’esprit abattu, qui le supportera?
15 Moyo wa mwenye akili hujipatia maarifa na usikivu wa mwenye busara huitafuta.
Le cœur de l’homme intelligent acquiert la connaissance, et l’oreille des sages cherche la connaissance.
16 Zawadi ya mtu inaweza kufungua njia na kumleta mbele ya mtu muhimu.
Le don d’un homme lui fait faire place et l’introduit devant les grands.
17 Wa kwanza kujitetea katika shitaka lake huonekana kuwa na haki hadi mpinzani wake aje na kumuuliza maswali.
Celui qui est le premier dans son procès est juste; son prochain vient, et l’examine.
18 Kupiga kura kunamaliza mabishano na kuwatawanya wapinzani imara.
Le sort fait cesser les querelles et sépare les puissants.
19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kushawishiwa kuliko mji wenye nguvu, na kugombana ni kama makomeo ya ngome.
Un frère offensé est plus [difficile] à gagner qu’une ville forte, et les querelles sont comme les verrous d’un palais.
20 Tumbo la mtu litashiba kutoka kwenye tunda la kinywa chake; atatoshelezwa kwa mavuno ya midomo yake.
Le ventre d’un homme est rassasié du fruit de sa bouche; du revenu de ses lèvres il est rassasié.
21 Uzima na kifo hutawaliwa kwa ulimi, na wale wenye kuupenda ulimi watakula tunda lake.
La mort et la vie sont au pouvoir de la langue, et celui qui l’aime mangera de son fruit.
22 Yeye apataye mke anapata kitu chema na kupokea fadhila kutoka kwa Yehova.
Celui qui a trouvé une femme a trouvé une bonne chose, et il a obtenu faveur de la part de l’Éternel.
23 Mtu masikini huomba rehema, lakini mtu tajiri hujibu kwa ukali.
Le pauvre parle en supplications, mais le riche répond des choses dures.
24 Anayejidai kwa marafiki wengi watamleta katika uharibifu, bali yupo rafiki ambaye huwa karibu kuliko ndugu.
L’homme qui a [beaucoup] de compagnons va se ruinant; mais il est tel ami plus attaché qu’un frère.