< Mithali 17 >

1 Ni bora kuwa na utulivu pamoja chembe za mkate kuliko nyumba yenye sherehe nyingi pamoja na ugomvi.
pleasant morsel dry and ease in/on/with her from house: home full sacrifice strife
2 Mtumishi mwenye busara atatawala juu ya mwana atendaye kwa aibu na atashiriki urithi kama mmoja wa ndugu.
servant/slave be prudent to rule in/on/with son: child be ashamed and in/on/with midst brother: male-sibling to divide inheritance
3 Kalibu ni kwa fedha na tanuu ni kwa dhahabu, bali Yehova huisafisha mioyo.
crucible to/for silver: money and furnace to/for gold and to test heart LORD
4 Mtu atendaye mabaya huwasikiliza wale wanaosema maovu; muongo anausikivu kwa wale wanaosema mambo mabaya.
be evil to listen upon lips evil: wickedness deception to listen upon tongue desire
5 Mwenye kumdhihaki masikini humtukana Muumba wake na anayefurahia msiba hatakosa adhabu.
to mock to/for be poor to taunt to make him glad to/for calamity not to clear
6 Wajukuu ni taji ya wazee na wazazi huleta heshima kwa watoto wao.
crown old son: descendant/people son: descendant/people and beauty son: child father their
7 Hotuba ya ushawishi haifai kwa mpumbavu; kidogo zaidi midomo ya uongo inafaa kwa ufalme.
not lovely to/for foolish lip: words remainder also for to/for noble lip: words deception
8 Rushwa ni kama jiwe la kiini macho kwa yule ambaye atoaye; yeye anayeiacha, hufanikiwa.
stone favor [the] bribe in/on/with eye master: owning his to(wards) all which to turn be prudent
9 Anayesamehe kosa hutafuta upendo, bali yeye anayerudia jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.
to cover transgression to seek love and to repeat in/on/with word: thing to separate tame
10 Karipio hupenya ndani ya mtu mwenye ufahamu kuliko mapigo mamia kwenda kwa mpumbavu.
to descend rebuke in/on/with to understand from to smite fool hundred
11 Mtu mbaya hutafuta uasi tu, hivyo mjumbe katiri atatumwa dhidi yake.
surely rebellion to seek bad: evil and messenger cruel to send: depart in/on/with him
12 Ni bora kukutana na dubu aliyeporwa watoto wake kuliko kukutana na mpumbavu katika upumbavu wake.
to meet bear childless in/on/with man and not fool in/on/with folly his
13 Mtu anaporudisha mabaya badala ya mema, mabaya hayatatoka katika nyumba yake.
to return: return distress: evil underneath: instead welfare not (to remove *Q(k)*) distress: evil from house: home his
14 Mwanzo wa mafarakano ni kama mtu anayefungulia maji kila mahali, hivyo ondoka kwenye mabishano kabla ya kutokea.
to separate water first: beginning strife and to/for face: before to quarrel [the] strife to leave
15 Yeye ambaye huwaachilia watu waovu au kuwalaumu wale wanaotenda haki - watu hawa wote ni chukizo kwa Yehova.
to justify wicked and be wicked righteous abomination LORD also two their
16 Kwa nini mpumbavu alipe fedha kwa kujifunza hekima, wakati hana uwezo wa kujifunza?
to/for what? this price in/on/with hand fool to/for to buy wisdom and heart nothing
17 Rafiki hupenda kwa nyakati zote na ndugu amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.
in/on/with all time to love: lover [the] neighbor and brother: male-sibling to/for distress to beget
18 Mtu asiyekuwa na akili hufanya ahadi zenye mashariti na kuanza kuwajibika kwa madeni ya jirani yake.
man lacking heart to blow palm to pledge pledge to/for face neighbor his
19 Apendaye mafarakano anapenda dhambi; ambaye hutengeneza kizingiti kirefu sana kwenye mlango wake husababisha kuvunjia kwa mifupa.
to love: lover transgression to love: lover strife to exult entrance his to seek breaking
20 Mtu mwenye moyo wa udanganyifu hapati chochote ambacho ni chema; na mwenye ulimi wa ukaidi huanguka kwenye janga.
twisted heart not to find good and to overturn in/on/with tongue his to fall: fall in/on/with distress: harm
21 Mzazi wa mpumbavu huleta majonzi kwake mwenyewe; baba wa mpumbavu hana furaha.
to beget fool to/for grief to/for him and not to rejoice father foolish
22 Moyo mchangamfu ni dawa njema, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
heart glad be good cure and spirit stricken to wither bone
23 Mtu mwovu hukubali rushwa ya siri ili kupotosha njia za haki.
bribe from bosom: secret wicked to take: recieve to/for to stretch way justice
24 Mwenye ufahamu huelekeza uso wake kwenye hekima, bali macho ya mpumbavu huelekea ncha za dunia.
with face to understand wisdom and eye fool in/on/with end land: country/planet
25 Mwana mpumbavu ni huzuni kwa baba yake na uchungu kwa mwanamke aliyemzaa.
vexation to/for father his son: child fool and bitterness to/for to beget him
26 Pia, si vizuri kumwadhibu mwenye kutenda haki; wala si vema kuwachapa mjeledi watu waadilifu wenye ukamilifu.
also to fine to/for righteous not pleasant to/for to smite noble upon uprightness
27 Mwenye maarifa hutumia maneno machache na mwenye ufahamu ni mtulivu.
to withhold word his to know knowledge (precious *Q(K)*) spirit: temper man understanding
28 Hata mpumbavu hudhaniwa kuwa na busara kama akikaa kimya; wakati anapokaa amefunga kinywa chake, anafikiriwa kuwa na akili.
also fool(ish) be quiet wise to devise: think to shutter lips his to understand

< Mithali 17 >