< Mithali 17 >

1 Ni bora kuwa na utulivu pamoja chembe za mkate kuliko nyumba yenye sherehe nyingi pamoja na ugomvi.
Bedre en tør Bid Brød med fred end Huset fuldt af Sul med Trætte.
2 Mtumishi mwenye busara atatawala juu ya mwana atendaye kwa aibu na atashiriki urithi kama mmoja wa ndugu.
Klog Træl bliver Herre over dårlig Søn og får lod og del mellem brødre.
3 Kalibu ni kwa fedha na tanuu ni kwa dhahabu, bali Yehova huisafisha mioyo.
Digel til Sølv og Ovn til Guld, men den, der prøver Hjerter, er HERREN.
4 Mtu atendaye mabaya huwasikiliza wale wanaosema maovu; muongo anausikivu kwa wale wanaosema mambo mabaya.
Den onde hører på onde Læber, Løgneren lytter til giftige Tunger.
5 Mwenye kumdhihaki masikini humtukana Muumba wake na anayefurahia msiba hatakosa adhabu.
Hvo Fattigmand spotter, håner hans Skaber, den skadefro slipper ikke for Straf.
6 Wajukuu ni taji ya wazee na wazazi huleta heshima kwa watoto wao.
De gamles Krone er Børnebørn, Sønners Stolthed er Fædre.
7 Hotuba ya ushawishi haifai kwa mpumbavu; kidogo zaidi midomo ya uongo inafaa kwa ufalme.
Ypperlig Tale er ej for en Dåre, end mindre da Løgnfor den, som er ædel.
8 Rushwa ni kama jiwe la kiini macho kwa yule ambaye atoaye; yeye anayeiacha, hufanikiwa.
Som en Troldsten er Gave i Giverens Øjne; hvorhen den end vender sig, gør den sin Virkning.
9 Anayesamehe kosa hutafuta upendo, bali yeye anayerudia jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.
Den, der dølger en Synd, søger Venskab, men den, der ripper op i en Sag, skiller Venner.
10 Karipio hupenya ndani ya mtu mwenye ufahamu kuliko mapigo mamia kwenda kwa mpumbavu.
Bedre virker Skænd på forstandig end hundrede Slag på en Tåbe.
11 Mtu mbaya hutafuta uasi tu, hivyo mjumbe katiri atatumwa dhidi yake.
Den onde har kun Genstridigbed for, men et skånselsløst Bud er udsendt imod ham.
12 Ni bora kukutana na dubu aliyeporwa watoto wake kuliko kukutana na mpumbavu katika upumbavu wake.
Man kan møde en Bjørn, hvis Unger er taget, men ikke en Tåbe udi hans Dårskab.
13 Mtu anaporudisha mabaya badala ya mema, mabaya hayatatoka katika nyumba yake.
Den, der gengælder godt med ondt, fra hans Hus skal Vanheld ej vige.
14 Mwanzo wa mafarakano ni kama mtu anayefungulia maji kila mahali, hivyo ondoka kwenye mabishano kabla ya kutokea.
At yppe Strid er at åbne for Vand, hold derfor inde, før Strid bryder løs.
15 Yeye ambaye huwaachilia watu waovu au kuwalaumu wale wanaotenda haki - watu hawa wote ni chukizo kwa Yehova.
At frikende skyldig og dømme uskyldig, begge Dele er HERREN en Gru.
16 Kwa nini mpumbavu alipe fedha kwa kujifunza hekima, wakati hana uwezo wa kujifunza?
Hvad hjælper Penge i Tåbens Hånd til at købe ham Visdom, når Viddet mangler?
17 Rafiki hupenda kwa nyakati zote na ndugu amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.
Ven viser Kærlighed når som helst, Broder fødes til Hjælp i Nød.
18 Mtu asiyekuwa na akili hufanya ahadi zenye mashariti na kuanza kuwajibika kwa madeni ya jirani yake.
Mand uden Vid giver Håndslag og går i Borgen for Næsten.
19 Apendaye mafarakano anapenda dhambi; ambaye hutengeneza kizingiti kirefu sana kwenye mlango wake husababisha kuvunjia kwa mifupa.
Ven af Kiv er Ven af Synd; at højne sin Dør er at attrå Fald.
20 Mtu mwenye moyo wa udanganyifu hapati chochote ambacho ni chema; na mwenye ulimi wa ukaidi huanguka kwenye janga.
Ej finder man Lykke, når Hjertet er vrangt, man falder i Våde, når Tungen er falsk.
21 Mzazi wa mpumbavu huleta majonzi kwake mwenyewe; baba wa mpumbavu hana furaha.
Den, der avler en Tåbe, får Sorg, Dårens Fader er ikke glad.
22 Moyo mchangamfu ni dawa njema, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
Glad Hjerte er godt for Legemet, nedslået Sind suger Marv af Benene.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa ya siri ili kupotosha njia za haki.
Den gudløse tager Gave i Løn for at bøje Rettens Gænge.
24 Mwenye ufahamu huelekeza uso wake kwenye hekima, bali macho ya mpumbavu huelekea ncha za dunia.
Visdom står den forstandige for Øje, Tåbens Blik er ved Jordens Ende.
25 Mwana mpumbavu ni huzuni kwa baba yake na uchungu kwa mwanamke aliyemzaa.
Tåbelig Søn er sin Faders Sorg, Kvide for hende, som fødte ham.
26 Pia, si vizuri kumwadhibu mwenye kutenda haki; wala si vema kuwachapa mjeledi watu waadilifu wenye ukamilifu.
At straffe den, der har Ret, er ilde, værre endnu at slå de ædle.
27 Mwenye maarifa hutumia maneno machache na mwenye ufahamu ni mtulivu.
Den, som har Kundskab tøjler sin Tale, Mand med Forstand er koldblodig.
28 Hata mpumbavu hudhaniwa kuwa na busara kama akikaa kimya; wakati anapokaa amefunga kinywa chake, anafikiriwa kuwa na akili.
Selv Dåren, der tier, gælder for viis, forstandig er den, der lukker sine Læber.

< Mithali 17 >