< Mithali 17 >

1 Ni bora kuwa na utulivu pamoja chembe za mkate kuliko nyumba yenye sherehe nyingi pamoja na ugomvi.
設筵滿屋,大家相爭, 不如有塊乾餅,大家相安。
2 Mtumishi mwenye busara atatawala juu ya mwana atendaye kwa aibu na atashiriki urithi kama mmoja wa ndugu.
僕人辦事聰明,必管轄貽羞之子, 又在眾子中同分產業。
3 Kalibu ni kwa fedha na tanuu ni kwa dhahabu, bali Yehova huisafisha mioyo.
鼎為煉銀,爐為煉金; 惟有耶和華熬煉人心。
4 Mtu atendaye mabaya huwasikiliza wale wanaosema maovu; muongo anausikivu kwa wale wanaosema mambo mabaya.
行惡的,留心聽奸詐之言; 說謊的,側耳聽邪惡之語。
5 Mwenye kumdhihaki masikini humtukana Muumba wake na anayefurahia msiba hatakosa adhabu.
戲笑窮人的,是辱沒造他的主; 幸災樂禍的,必不免受罰。
6 Wajukuu ni taji ya wazee na wazazi huleta heshima kwa watoto wao.
子孫為老人的冠冕; 父親是兒女的榮耀。
7 Hotuba ya ushawishi haifai kwa mpumbavu; kidogo zaidi midomo ya uongo inafaa kwa ufalme.
愚頑人說美言本不相宜, 何況君王說謊話呢?
8 Rushwa ni kama jiwe la kiini macho kwa yule ambaye atoaye; yeye anayeiacha, hufanikiwa.
賄賂在餽送的人眼中看為寶玉, 隨處運動都得順利。
9 Anayesamehe kosa hutafuta upendo, bali yeye anayerudia jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.
遮掩人過的,尋求人愛; 屢次挑錯的,離間密友。
10 Karipio hupenya ndani ya mtu mwenye ufahamu kuliko mapigo mamia kwenda kwa mpumbavu.
一句責備話深入聰明人的心, 強如責打愚昧人一百下。
11 Mtu mbaya hutafuta uasi tu, hivyo mjumbe katiri atatumwa dhidi yake.
惡人只尋背叛, 所以必有嚴厲的使者奉差攻擊他。
12 Ni bora kukutana na dubu aliyeporwa watoto wake kuliko kukutana na mpumbavu katika upumbavu wake.
寧可遇見丟崽子的母熊, 不可遇見正行愚妄的愚昧人。
13 Mtu anaporudisha mabaya badala ya mema, mabaya hayatatoka katika nyumba yake.
以惡報善的, 禍患必不離他的家。
14 Mwanzo wa mafarakano ni kama mtu anayefungulia maji kila mahali, hivyo ondoka kwenye mabishano kabla ya kutokea.
紛爭的起頭如水放開, 所以,在爭鬧之先必當止息爭競。
15 Yeye ambaye huwaachilia watu waovu au kuwalaumu wale wanaotenda haki - watu hawa wote ni chukizo kwa Yehova.
定惡人為義的,定義人為惡的, 這都為耶和華所憎惡。
16 Kwa nini mpumbavu alipe fedha kwa kujifunza hekima, wakati hana uwezo wa kujifunza?
愚昧人既無聰明, 為何手拿價銀買智慧呢?
17 Rafiki hupenda kwa nyakati zote na ndugu amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.
朋友乃時常親愛, 弟兄為患難而生。
18 Mtu asiyekuwa na akili hufanya ahadi zenye mashariti na kuanza kuwajibika kwa madeni ya jirani yake.
在鄰舍面前擊掌作保 乃是無知的人。
19 Apendaye mafarakano anapenda dhambi; ambaye hutengeneza kizingiti kirefu sana kwenye mlango wake husababisha kuvunjia kwa mifupa.
喜愛爭競的,是喜愛過犯; 高立家門的,乃自取敗壞。
20 Mtu mwenye moyo wa udanganyifu hapati chochote ambacho ni chema; na mwenye ulimi wa ukaidi huanguka kwenye janga.
心存邪僻的,尋不着好處; 舌弄是非的,陷在禍患中。
21 Mzazi wa mpumbavu huleta majonzi kwake mwenyewe; baba wa mpumbavu hana furaha.
生愚昧子的,必自愁苦; 愚頑人的父毫無喜樂。
22 Moyo mchangamfu ni dawa njema, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
喜樂的心乃是良藥; 憂傷的靈使骨枯乾。
23 Mtu mwovu hukubali rushwa ya siri ili kupotosha njia za haki.
惡人暗中受賄賂, 為要顛倒判斷。
24 Mwenye ufahamu huelekeza uso wake kwenye hekima, bali macho ya mpumbavu huelekea ncha za dunia.
明哲人眼前有智慧; 愚昧人眼望地極。
25 Mwana mpumbavu ni huzuni kwa baba yake na uchungu kwa mwanamke aliyemzaa.
愚昧子使父親愁煩, 使母親憂苦。
26 Pia, si vizuri kumwadhibu mwenye kutenda haki; wala si vema kuwachapa mjeledi watu waadilifu wenye ukamilifu.
刑罰義人為不善; 責打君子為不義。
27 Mwenye maarifa hutumia maneno machache na mwenye ufahamu ni mtulivu.
寡少言語的,有知識; 性情溫良的,有聰明。
28 Hata mpumbavu hudhaniwa kuwa na busara kama akikaa kimya; wakati anapokaa amefunga kinywa chake, anafikiriwa kuwa na akili.
愚昧人若靜默不言也可算為智慧; 閉口不說也可算為聰明。

< Mithali 17 >