< Mithali 16 >

1 Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
W człowieku są zamysły serca, ale odpowiedź języka jest od PANA.
2 Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
Wszystkie drogi człowieka są czyste w jego oczach, ale PAN waży duchy.
3 Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
Powierz PANU swe dzieła, a twoje zamysły będą utwierdzone.
4 Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
PAN uczynił wszystko dla samego siebie, nawet niegodziwego na dzień zła.
5 Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
Każdy, który jest wyniosłego serca, budzi odrazę w PANU; choć weźmie innych do pomocy, nie uniknie kary.
6 Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
Dzięki miłosierdziu i prawdzie oczyszcza się nieprawość, a w bojaźni PANA oddalamy się od zła.
7 Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
Gdy drogi człowieka podobają się PANU, to godzi z nim nawet jego nieprzyjaciół.
8 Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
Lepiej mieć mało ze sprawiedliwością niż wiele dochodów nieprawnych.
9 Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
Serce człowieka obmyśla swe drogi, ale PAN kieruje jego krokami.
10 Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
Wyrok Boży [jest] na wargach króla; jego usta nie błądzą w sądzie.
11 Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
Sprawiedliwa waga i szale [należą do] PANA i wszystkie odważniki w worku są jego dziełem.
12 Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
Popełnienie niegodziwości budzi odrazę w królach, bo sprawiedliwością tron jest umocniony.
13 Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
Wargi sprawiedliwe są rozkoszą królów, kochają oni tego, który mówi to, co słuszne.
14 Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
Gniew króla jest posłańcem śmierci, ale mądry człowiek przebłaga go.
15 Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
W jasności twarzy króla [jest] życie, a jego przychylność jest jak obłok z późnym deszczem.
16 Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
O wiele lepiej jest nabyć mądrość niż złoto; a nabyć rozum lepiej niż srebro.
17 Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
Droga prawych [to] odstąpić od zła; kto strzeże swojej drogi, strzeże swej duszy.
18 Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
Pycha poprzedza zgubę, a wyniosły duch – upadek.
19 Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
Lepiej być uniżonego ducha z pokornymi, niż dzielić łup z pysznymi.
20 Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
Kto zważa na słowo, znajdzie dobro, a kto ufa PANU, [jest] błogosławiony.
21 Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
Kto [jest] mądrego serca, zwie się rozumnym, a słodycz warg pomnaża wiedzę.
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
Rozum [jest] zdrojem życia dla tych, którzy go mają, a pouczenie głupich jest głupotą.
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
Serce mądrego czyni jego usta roztropnymi i dodaje nauki jego wargom.
24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
Miłe słowa są [jak] plaster miodu, słodycz dla duszy i lekarstwo dla kości.
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
Jest droga, która [wydaje się] człowiekowi słuszna, ale jej końcem jest droga do śmierci.
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
Robotnik pracuje dla siebie, bo usta pobudzają go [do tego].
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
Człowiek nikczemny wykopuje zło, a na jego wargach jakby ogień płonący.
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
Człowiek przewrotny rozsiewa spory, a plotkarz rozdziela przyjaciół.
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
Człowiek gwałtowny zwabia swego bliźniego i wprowadza go na drogę niedobrą.
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
Mruga swymi oczami, by knuć podstępy; rusza wargami i popełnia zło.
31 Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
Siwa głowa [jest] koroną chwały, zdobywa się ją na drodze sprawiedliwości.
32 Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
Lepszy jest nieskory do gniewu niż mocarz, a kto panuje nad swym duchem, [jest lepszy] niż ten, kto zdobywa miasto.
33 Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.
Losy wrzuca się w zanadrze, ale całe rozstrzygnięcie ich zależy od PANA.

< Mithali 16 >