< Mithali 16 >

1 Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
hominis est animum praeparare et Dei gubernare linguam
2 Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
omnes viae hominum patent oculis eius spirituum ponderator est Dominus
3 Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
revela Domino opera tua et dirigentur cogitationes tuae
4 Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
universa propter semet ipsum operatus est Dominus impium quoque ad diem malum
5 Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
abominatio Domini omnis arrogans etiam si manus ad manum fuerit non erit innocens
6 Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
misericordia et veritate redimitur iniquitas et in timore Domini declinatur a malo
7 Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
cum placuerint Domino viae hominis inimicos quoque eius convertet ad pacem
8 Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
melius est parum cum iustitia quam multi fructus cum iniquitate
9 Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
cor hominis disponet viam suam sed Domini est dirigere gressus eius
10 Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
divinatio in labiis regis in iudicio non errabit os eius
11 Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
pondus et statera iudicia Domini sunt et opera eius omnes lapides sacculi
12 Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
abominabiles regi qui agunt impie quoniam iustitia firmatur solium
13 Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
voluntas regum labia iusta qui recta loquitur diligetur
14 Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
indignatio regis nuntii mortis et vir sapiens placabit eam
15 Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
in hilaritate vultus regis vita et clementia eius quasi imber serotinus
16 Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
posside sapientiam quia auro melior est et adquire prudentiam quia pretiosior est argento
17 Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
semita iustorum declinat mala custos animae suae servat viam suam
18 Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
contritionem praecedit superbia et ante ruinam exaltatur spiritus
19 Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
melius est humiliari cum mitibus quam dividere spolia cum superbis
20 Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
eruditus in verbo repperiet bona et qui in Domino sperat beatus est
21 Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
qui sapiens corde est appellabitur prudens et qui dulcis eloquio maiora percipiet
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
fons vitae eruditio possidentis doctrina stultorum fatuitas
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
cor sapientis erudiet os eius et labiis illius addet gratiam
24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
favus mellis verba conposita dulcedo animae et sanitas ossuum
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
est via quae videtur homini recta et novissimum eius ducit ad mortem
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
anima laborantis laborat sibi quia conpulit eum os suum
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
vir impius fodit malum et in labiis eius ignis ardescit
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
homo perversus suscitat lites et verbosus separat principes
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
vir iniquus lactat amicum suum et ducit eum per viam non bonam
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
qui adtonitis oculis cogitat prava mordens labia sua perficit malum
31 Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
corona dignitatis senectus in viis iustitiae repperietur
32 Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
melior est patiens viro forte et qui dominatur animo suo expugnatore urbium
33 Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.
sortes mittuntur in sinu sed a Domino temperantur

< Mithali 16 >