< Mithali 16 >

1 Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
לאדם מערכי-לב ומיהוה מענה לשון
2 Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
כל-דרכי-איש זך בעיניו ותכן רוחות יהוה
3 Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
גל אל-יהוה מעשיך ויכנו מחשבתיך
4 Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
כל פעל יהוה למענהו וגם-רשע ליום רעה
5 Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
תועבת יהוה כל-גבה-לב יד ליד לא ינקה
6 Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
בחסד ואמת יכפר עון וביראת יהוה סור מרע
7 Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
ברצות יהוה דרכי-איש גם-אויביו ישלם אתו
8 Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
טוב-מעט בצדקה-- מרב תבואות בלא משפט
9 Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
לב אדם יחשב דרכו ויהוה יכין צעדו
10 Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
קסם על-שפתי-מלך במשפט לא ימעל-פיו
11 Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
פלס ומאזני משפט--ליהוה מעשהו כל-אבני-כיס
12 Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
תועבת מלכים עשות רשע כי בצדקה יכון כסא
13 Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
רצון מלכים שפתי-צדק ודבר ישרים יאהב
14 Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
חמת-מלך מלאכי-מות ואיש חכם יכפרנה
15 Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
באור-פני-מלך חיים ורצונו כעב מלקוש
16 Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
קנה-חכמה--מה-טוב מחרוץ וקנות בינה נבחר מכסף
17 Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
מסלת ישרים סור מרע שמר נפשו נצר דרכו
18 Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
לפני-שבר גאון ולפני כשלון גבה רוח
19 Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
טוב שפל-רוח את-עניים (ענוים) מחלק שלל את-גאים
20 Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
משכיל על-דבר ימצא-טוב ובוטח ביהוה אשריו
21 Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
לחכם-לב יקרא נבון ומתק שפתים יסיף לקח
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
מקור חיים שכל בעליו ומוסר אולים אולת
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
לב חכם ישכיל פיהו ועל-שפתיו יסיף לקח
24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
צוף-דבש אמרי-נעם מתוק לנפש ומרפא לעצם
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
יש דרך ישר לפני-איש ואחריתה דרכי-מות
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
נפש עמל עמלה לו כי-אכף עליו פיהו
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
איש בליעל כרה רעה ועל-שפתיו (שפתו) כאש צרבת
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
איש תהפכות ישלח מדון ונרגן מפריד אלוף
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
איש חמס יפתה רעהו והוליכו בדרך לא-טוב
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
עצה עיניו לחשב תהפכות קרץ שפתיו כלה רעה
31 Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
עטרת תפארת שיבה בדרך צדקה תמצא
32 Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
טוב ארך אפים מגבור ומשל ברוחו מלכד עיר
33 Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.
בחיק יוטל את-הגורל ומיהוה כל-משפטו

< Mithali 16 >