< Mithali 16 >

1 Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
Les préparations du cœur sont à l'homme; mais le discours de la langue est de par l'Eternel.
2 Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
Chacune des voies de l'homme lui semble pure; mais l'Eternel pèse les esprits.
3 Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
Remets tes affaires à l'Eternel, et tes pensées seront bien ordonnées.
4 Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
L'Eternel a fait tout pour soi-même; et même le méchant pour le jour de la calamité.
5 Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
L'Eternel a en abomination tout homme hautain de cœur; de main en main il ne demeurera point impuni.
6 Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
Il y aura propitiation pour l'iniquité par la miséricorde et la vérité; et on se détourne du mal par la crainte de l'Eternel.
7 Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
Quand l'Eternel prend plaisir aux voies de l'homme, il apaise envers lui ses ennemis mêmes.
8 Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
Il vaut mieux un peu de bien avec justice, qu'un gros revenu là où l'on n'a point de droit.
9 Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
Le cœur de l'homme délibère de sa voie; mais l'Eternel conduit ses pas.
10 Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
Il y a divination aux lèvres du Roi, et sa bouche ne se fourvoiera point du droit.
11 Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
La balance et le trébuchet justes sont de l'Eternel, et tous les poids du sachet sont son œuvre.
12 Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
Ce doit être une abomination aux Rois de faire injustice, parce que le trône est établi par la justice.
13 Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
Les Rois [doivent prendre] plaisir aux lèvres de justice, et aimer celui qui profère des choses justes.
14 Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
Ce sont autant de messagers de mort que la colère du Roi; mais l'homme sage l'apaisera.
15 Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
C'est vie que le visage serein du Roi, et sa faveur est comme la nuée portant la pluie de la dernière saison.
16 Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
Combien est-il plus précieux que le fin or, d'acquérir de la sagesse; et combien est-il plus excellent que l'argent, d'acquérir de la prudence?
17 Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
Le chemin relevé des hommes droits, c'est de se détourner du mal; celui-là garde son âme qui prend garde à son train.
18 Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
L'orgueil va devant l'écrasement; et la fierté d'esprit devant la ruine.
19 Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
Mieux vaut être humilié d'esprit avec les débonnaires, que de partager le butin avec les orgueilleux.
20 Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
Celui qui prend garde à la parole, trouvera le bien; et celui qui se confie en l'Eternel, est bienheureux.
21 Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
On appellera prudent le sage de cœur; et la douceur des lèvres augmente la doctrine.
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
La prudence est à ceux qui la possèdent une source de vie; mais l'instruction des fous est une folie.
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
Le cœur sage conduit prudemment sa bouche, et ajoute doctrine sur ses lèvres.
24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
Les paroles agréables sont des rayons de miel, douceur à l'âme, et santé aux os.
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
II y a telle voie qui semble droite à l'homme, mais dont la fin sont les voies de la mort.
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
L'âme de celui qui travaille, travaille pour lui-même, parce que sa bouche se courbe devant lui.
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
Le méchant creuse le mal, et il y a comme un feu brûlant sur ses lèvres.
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
L'homme qui use de renversements, sème des querelles, et le rapporteur met le plus grand ami en division.
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
L'homme violent attire son compagnon, et le fait marcher par une voie qui n'est pas bonne.
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
Il fait signe des yeux pour machiner des renversements, et remuant ses lèvres il exécute le mal.
31 Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
Les cheveux blancs sont une couronne d'honneur; et elle se trouvera dans la voie de la justice.
32 Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
Celui qui est tardif à colère, vaut mieux que l'homme fort; et celui qui est le maître de son cœur, vaut mieux que celui qui prend des villes.
33 Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.
On jette le sort au giron, mais tout ce qui en doit arriver, est de par l'Eternel.

< Mithali 16 >