< Mithali 16 >

1 Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
To man belongeth the preparation of the heart; But the answer of the tongue is from the LORD.
2 Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
All the ways of a man are pure in his own eyes; But the LORD weigheth the spirit.
3 Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
Commit thy doings to the LORD, And thy purposes shall be established.
4 Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
The LORD hath ordained every thing for its end; Yea, even the wicked for the day of evil.
5 Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
Every one that is proud in heart is an abomination to the LORD; From generation to generation he shall not be unpunished.
6 Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
Through kindness and truth, iniquity is expiated; And, through the fear of the LORD, men depart from evil.
7 Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
When a man's ways please the LORD, He maketh even his enemies to be at peace with him.
8 Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
Better is a little with righteousness, Than great revenues without right.
9 Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
The heart of man deviseth his way, But the LORD establisheth his steps.
10 Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
A divine sentence is upon the lips of a king; His mouth transgresseth not in judgment.
11 Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
A just balance and scales are the appointment of the LORD; All the weights of the bag are his work.
12 Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
The doing of wickedness is an abomination to kings; For by righteousness is the throne established.
13 Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
Righteous lips are the delight of kings, And they love him who speaketh right things.
14 Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
The wrath of a king is messengers of death; But a wise man will pacify it.
15 Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
In the light of the king's countenance is life, And his favor is a like a cloud bringing the latter rain.
16 Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
How much better is it to get wisdom than gold! Yea, to get understanding is rather to be chosen than silver.
17 Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
It is the highway of the upright to depart from evil; He that taketh heed to his way preserveth his life.
18 Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
Pride goeth before destruction, And a haughty spirit before a fall.
19 Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
Better is it to be of a humble spirit with the lowly, Than to share the spoil with the proud.
20 Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
He who giveth heed to the word shall find good; And he who trusteth in the LORD, happy is he!
21 Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
The wise in heart shall be called intelligent, And sweetness of the lips increaseth learning.
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
Understanding is a wellspring of life to him that hath it. And the chastisement of fools is their folly.
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
The heart of the wise man instructeth his mouth, And addeth learning to his lips.
24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
Pleasant words are like a honeycomb, Sweet to the taste, and health to the bones.
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
There is a way that seemeth right to a man, But the end thereof is the way to death.
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
The hunger of the laborer laboreth for him; For his mouth urgeth him on.
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
A worthless man diggeth mischief, And on his lips there is, as it were, a burning fire.
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
A deceitful man stirreth up strife, And a whisperer separateth friends.
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
A man of violence enticeth his neighbor, And leadeth him into a way which is not good.
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
He who shutteth his eyes to devise fraud, He who compresseth his lips, hath accomplished mischief!
31 Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
The hoary head is a crown of glory, If it be found in the way of righteousness.
32 Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
He who is slow to anger is better than the mighty; And he who ruleth his spirit, than he that taketh a city.
33 Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.
The lot is cast into the lap; But the whole decision thereof is from the LORD.

< Mithali 16 >