< Mithali 16 >

1 Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
Arrangements of the heart [are] of man, An answer of the tongue from YHWH.
2 Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
All the ways of a man are pure in his own eyes, And YHWH is pondering the spirits.
3 Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
Roll your works to YHWH, And your purposes are established,
4 Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
YHWH has worked all things for Himself, And also the wicked—for a day of evil.
5 Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
Every proud one of heart [is] an abomination to YHWH, Hand to hand—he is not acquitted.
6 Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
Iniquity is pardoned in kindness and truth, And in the fear of YHWH Turn aside from evil.
7 Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
When a man’s ways please YHWH, even his enemies, He causes to be at peace with him.
8 Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
Better [is] a little with righteousness, Than abundance of increase without justice.
9 Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
The heart of man devises his way, And YHWH establishes his step.
10 Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
An oath [is] on the lips of a king, In judgment his mouth does not trespass.
11 Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
A just beam and balances [are] YHWH’s, All the stones of the bag [are] His work.
12 Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
Doing wickedness [is] an abomination to kings, For a throne is established by righteousness.
13 Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
Righteous lips [are] the delight of kings, And he loves whoever is speaking uprightly,
14 Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
The fury of a king [is] messengers of death, And a wise man pacifies it.
15 Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
In the light of a king’s face [is] life, And his goodwill [is] as a cloud of the spring rain.
16 Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
To get wisdom—how much better than gold, And to get understanding—to be chosen [more] than silver!
17 Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
A highway of the upright [is] to turn from evil, Whoever is preserving his soul is watching his way.
18 Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
Pride [is] before destruction, And before stumbling—a haughty spirit.
19 Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
Better is humility of spirit with the poor, Than to apportion spoil with the proud.
20 Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
The wise in any matter finds good, And whoever is trusting in YHWH, O his blessedness.
21 Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
For the wise in heart is called intelligent, And sweetness of lips increases learning.
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
Understanding [is] a fountain of life to its possessors, The instruction of fools is folly.
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
The heart of the wise causes his mouth to act wisely, And he increases learning by his lips,
24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
Sayings of pleasantness [are] a honeycomb, Sweet to the soul, and healing to the bone.
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
There is a way right before a man, And its latter end—ways of death.
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
A laboring man has labored for himself, For his mouth has caused [him] to bend over it.
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
A worthless man is preparing evil, And on his lips [is] as a burning fire.
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
A contrary man sends forth contention, A tale-bearer is separating a familiar friend.
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
A violent man entices his neighbor, And causes him to go in a way [that is] not good.
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
Consulting his eyes to devise contrary things, Moving his lips he has accomplished evil.
31 Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
Grey hairs [are] a crown of beauty, It is found in the way of righteousness.
32 Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
Better [is] the [one] slow to anger than the mighty, And the ruler over his spirit than he who is taking a city.
33 Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.
The lot is cast into the center, And all its judgment [is] from YHWH!

< Mithali 16 >