< Mithali 16 >

1 Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
It is for man to prepare the soul, and for the Lord to govern the tongue.
2 Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
All the ways of a man are open to his eyes; the Lord is the one who weighs spirits.
3 Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
Open your works to the Lord, and your intentions will be set in order.
4 Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
The Lord has wrought all things because of himself. Likewise the impious is for the evil day.
5 Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
All the arrogant are an abomination to the Lord. Even if hand will be joined to hand, he is not innocent. The beginning of a good way is to do justice. And this is more acceptable with God than to immolate sacrifices.
6 Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
By mercy and truth, iniquity is redeemed. And by the fear of the Lord, one turns away from evil.
7 Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
When the ways of man will please the Lord, he will convert even his enemies to peace.
8 Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
Better is a little with justice, than many fruits with iniquity.
9 Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
The heart of man disposes his way. But it is for Lord to direct his steps.
10 Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
Foreknowledge is in the lips of the king. His mouth shall not err in judgment.
11 Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
Weights and scales are judgments of the Lord. And all the stones in the bag are his work.
12 Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
Those who act impiously are abominable to the king. For the throne is made firm by justice.
13 Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
Just lips are the will of kings. He who speaks honestly shall be loved.
14 Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
The indignation of a king is a herald of death. And the wise man will appease it.
15 Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
In the cheerfulness of the king’s countenance, there is life. And his clemency is like belated rain.
16 Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
Possess wisdom, for it is better than gold. And acquire prudence, for it is more precious than silver.
17 Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
The path of the just turns away from evils. He who guards his soul preserves his way.
18 Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
Arrogance precedes destruction. And the spirit is exalted before a fall.
19 Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
It is better to be humbled with the meek, than to divide spoils with the arrogant.
20 Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
The learned in word shall find good things. And whoever hopes in the Lord is blessed.
21 Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
Whoever is wise in heart shall be called prudent. And whoever is sweet in eloquence shall attain to what is greater.
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
Learning is a fountain of life to one who possesses it. The doctrine of the foolish is senseless.
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
The heart of the wise shall instruct his mouth and add grace to his lips.
24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
Careful words are a honeycomb: sweet to the soul and healthful to the bones.
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
There is a way which seems right to a man, and its end result leads to death.
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
The soul of the laborer labors for himself, because his mouth has driven him to it.
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
The impious man digs up evil, and in his lips is a burning fire.
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
A perverse man stirs up lawsuits. And one who is verbose divides leaders.
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
A man of iniquity entices his friend, and he leads him along a way that is not good.
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
Whoever, with astonished eyes, thinks up depravities, biting his lips, accomplishes evil.
31 Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
Old age is a crown of dignity, when it is found in the ways of justice.
32 Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
A patient man is better than a strong one. And whoever rules his soul is better than one who assaults cities.
33 Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.
Lots are cast into the lap, but they are tempered by the Lord.

< Mithali 16 >