< Mithali 16 >
1 Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
Čovjek snuje u srcu, a od Jahve je što će jezik odgovoriti.
2 Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
Čovjeku se svi njegovi putovi čine čisti, a Jahve ispituje duhove.
3 Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
Prepusti Jahvi svoja djela, i tvoje će se namisli ostvariti.
4 Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
Jahve je sve stvorio u svoju svrhu, pa i opakoga za dan zli.
5 Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
Mrzak je Jahvi svatko ohola duha: takav zaista ne ostaje bez kazne.
6 Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
Ljubavlju se i vjernošću pomiruje krivnja, i strahom se Gospodnjim uklanja zlo.
7 Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
Kad su Jahvi mili putovi čovječji, i neprijatelje njegove miri s njim.
8 Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
Bolje je malo s pravednošću nego veliki dohoci s nepravdom.
9 Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
Srce čovječje smišlja svoj put, ali Jahve upravlja korake njegove.
10 Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
Proročanstvo je na usnama kraljevim: u osudi se njegova usta neće ogriješiti.
11 Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
Mjere i tezulje pripadaju Jahvi; njegovo su djelo i svi utezi.
12 Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
Mrsko je kraljevima počiniti opačinu, jer se pravdom utvrđuje prijestolje.
13 Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
Mile su kraljevima usne pravedne i oni ljube onog koji govori pravo.
14 Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
Jarost je kraljeva vjesnik smrti ali je mudar čovjek ublaži.
15 Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
U kraljevu je vedru licu život, i njegova je milost kao oblak s kišom proljetnom.
16 Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
Probitačnije je steći mudrost nego zlato, i stjecati razbor dragocjenije je nego srebro.
17 Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
Životni je put pravednih: kloniti se zla, i tko pazi na svoj put, čuva život svoj.
18 Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
Pred slomom ide oholost i pred padom uznositost.
19 Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
Bolje je biti krotak s poniznima nego dijeliti plijen s oholima.
20 Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
Tko pazi na riječ, nalazi sreću, i tko se uzda u Jahvu, blago njemu.
21 Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
Mudar srcem naziva se razumnim i prijazne usne uvećavaju znanje.
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
Izvor je životni razum onima koji ga imaju, a ludima je kazna njihova ludost.
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
Mudračev duh urazumljuje usta njegova, na usnama mu znanje umnožava.
24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
Saće meda riječi su ljupke, slatke duši i lijek kostima.
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
Neki se put čini čovjeku prav, a na kraju vodi k smrti.
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
Radnikova glad radi za nj; jer ga tjeraju usta njegova.
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
Bezočnik pripravlja samo zlo i na usnama mu je oganj plameni.
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
Himben čovjek zameće svađu i klevetnik razdor među prijatelje.
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
Nasilnik zavodi bližnjega svoga i navodi ga na rđav put.
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
Tko očima namiguje, himbu smišlja, a tko usne stišće, već je smislio pakost.
31 Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
Sijede su kose prekrasna kruna, nalaze se na putu pravednosti.
32 Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
Tko se teško srdi, bolji je od junaka, i tko nad sobom vlada, bolji je od osvojitelja grada.
33 Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.
U krilo plašta baca se kocka, ali je od Jahve svaka odluka.