< Mithali 15 >

1 Jawabu la upole huondoa ghadhabu, bali neno la ukatili huchochea hasira.
Une réponse douce calme la fureur, mais une parole dure excite la colère.
2 Ulimi wa watu mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha wapumbavu humwaga upuuzi.
La langue des sages rend la science aimable; de la bouche des insensés déborde la folie.
3 Macho ya Yehova yapo kila mahali, yakiwatazama juu ya waovu na wema.
Les yeux de Yahweh sont en tout lieu, observant les méchants et les bons.
4 Ulimi unaoponya ni mti wa uzima, bali ulimi wa udanganyifu huvunja moyo.
la parole douce est un arbre de vie, mais la langue perverse brise le cœur.
5 Mpumbavu hudharau marudi ya baba yake, bali yeye anayejifunza kutokana na masahihisho ni mwenye hekima.
L’insensé méprise l’instruction de son père, mais celui qui profite de la réprimande devient plus sage.
6 Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
Il y a grande richesse dans la maison du juste, mais il y a du trouble dans les gains du méchant.
7 Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
Les lèvres du sage répandent la science, mais non le cœur de l’insensé.
8 Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.
Le sacrifice des méchants est en horreur à Yahweh, mais la prière des hommes droits lui plaît.
9 Yehova anachukia njia ya watu waovu, bali anampenda yule ambaye huandama haki.
La voie du méchant est en abomination à Yahweh, mais il aime celui qui poursuit la justice.
10 Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
Une correction sévère frappe celui qui abandonne le sentier; celui qui hait la réprimande mourra.
11 Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu? (Sheol h7585)
Le schéol et l’abîme sont à nu devant Yahweh: combien plus les cœurs des enfants des hommes! (Sheol h7585)
12 Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
Le moqueur n’aime pas qu’on le reprenne, il ne va pas vers les sages.
13 Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
Un cœur joyeux rend le visage serein, mais, quand le cœur est triste, l’esprit est abattu.
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.
Le cœur intelligent cherche la science, mais la bouche des insensés se repaît de folie.
15 Siku zote za watu waliokandamizwa ni taabu, bali moyo wenye furaha unakaramu daima.
Tous les jours de l’affligé sont mauvais, mais le cœur content est un festin perpétuel.
16 Bora kitu kidogo pamoja na kumcha Mungu kuliko hazina kubwa pamoja na ghasia.
Mieux vaut peu avec la crainte de Yahweh, qu’un grand trésor avec le trouble.
17 Bora mlo wenye mboga kukiwa na upendo kuliko kuandaliwa ndama aliyenona kwa chuki.
Mieux vaut des légumes avec de l’affection, qu’un bœuf gras avec de la haine.
18 Mtu mwenye hasira huchochea mabishano, bali mtu ambaye hukawia kukasirika hutuliza ugomvi.
L’homme violent excite des querelles, mais le patient apaise les disputes.
19 Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
Le chemin du paresseux est comme une haie d’épines, mais le sentier des hommes droits est aplani.
20 Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
Un fils sage fait la joie de son père, et l’insensé méprise sa mère.
21 Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
La folie est une joie pour l’homme dépourvu de sens, mais un homme intelligent suit le droit chemin.
22 Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
Les projets échouent faute de délibération, mais ils réussissent quand il y a de nombreux conseillers.
23 Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
L’homme a de la joie pour une bonne réponse de sa bouche, et combien est agréable une parole dite à propos!
24 Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu. (Sheol h7585)
Le sage suit un sentier de vie qui mène en haut, pour se détourner du schéol qui est en bas. (Sheol h7585)
25 Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
Yahweh renverse la maison des orgueilleux, mais il affermit les bornes de la veuve.
26 Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
Les pensées mauvaises sont en horreur à Yahweh, mais les paroles bienveillantes sont pures à ses yeux.
27 Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
Celui qui est âpre au gain trouble sa maison, mais celui qui hait les présents vivra.
28 Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
Le cœur du juste médite ce qu’il doit répondre, mais le mal jaillit de la bouche des méchants.
29 Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
Yahweh est loin des méchants, mais il écoute la prière des justes.
30 Nuru ya macho huleta furaha moyoni na habari njema ni afya kwenye mwili.
Un regard bienveillant réjouit le cœur; une bonne nouvelle engraisse les os.
31 Kama utazingatia wakati mtu anapokurekebisha jinsi ya kuishi, utabaki miongoni mwa watu wenye busara.
L’oreille qui écoute les réprimandes salutaires a sa demeure parmi les sages.
32 Yeye anayekataa karipio hujidharau mwenyewe, bali yule asikilizaye masahihisho hujipatia ufahamu.
Celui qui rejette la correction méprise son âme, mais celui qui écoute la réprimande acquiert la sagesse.
33 Kumcha Yehova hufundisha hekima na unyenyekevu huja kabla ya heshima.
La crainte de Yahweh est l’école de la sagesse, et l’humilité précède la gloire.

< Mithali 15 >