< Mithali 15 >
1 Jawabu la upole huondoa ghadhabu, bali neno la ukatili huchochea hasira.
Suloinen vastaus hillitse vihan, mutta kova sana saattaa mielen karvaaksi.
2 Ulimi wa watu mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha wapumbavu humwaga upuuzi.
Viisasten kieli saattaa opetuksen suloiseksi, vaan tyhmäin suu aina hulluuta sylkee.
3 Macho ya Yehova yapo kila mahali, yakiwatazama juu ya waovu na wema.
Herran silmät katselevat joka paikassa, sekä pahat että hyvät.
4 Ulimi unaoponya ni mti wa uzima, bali ulimi wa udanganyifu huvunja moyo.
Terveellinen kieli on elämän puu: vaan valhettelevainen saattaa sydämen kivun.
5 Mpumbavu hudharau marudi ya baba yake, bali yeye anayejifunza kutokana na masahihisho ni mwenye hekima.
Tyhmä laittaa isänsä kurituksen; vaan joka rangaistuksen ottaa, hän tulee taitavaksi.
6 Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
Vanhurskaan huoneessa on yltäkyllä; vaan jumalattoman saalis on hävintö.
7 Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
Viisasten huulet jakavat neuvoa; vaan tyhmäin sydän ei ole niin.
8 Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.
Jumalattoman uhri on Herralle kauhistus; vaan jumalisten rukous on hänelle otollinen.
9 Yehova anachukia njia ya watu waovu, bali anampenda yule ambaye huandama haki.
Jumalattoman tie on Herralle kauhistus; vaan joka vanhursjautta noudattaa, on hänelle rakas.
10 Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
Kuritus on sille paha, joka hylkää tiensä: ja joka rangaistusta vihaa, hänen pitää kuoleman.
11 Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu? (Sheol )
Helvetti ja kadotus on Herran edessä: kunka paljon enemmin ihmisten lasten sydämet. (Sheol )
12 Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
Ei pilkkaaja rakasta sitä, joka häntä rankaisee, ja ei hän mene viisasten tykö.
13 Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
Iloinen sydän tekee iloiset kasvot; vaan koska sydän on surullinen, niin rohkeus raukee.
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.
Ymmärtäväinen sydän etsii viisautta; vaan tyhmäin suu tyhmyydellä ravitaan.
15 Siku zote za watu waliokandamizwa ni taabu, bali moyo wenye furaha unakaramu daima.
Surullisella ihmisellä ei ole koskaan hyvää päivää; vaan jolla hyvä sydän on, hänellä on joka päivä vieraspito.
16 Bora kitu kidogo pamoja na kumcha Mungu kuliko hazina kubwa pamoja na ghasia.
Parempi on vähä Herran pelvossa, kuin suuri tavara ilman lepoa.
17 Bora mlo wenye mboga kukiwa na upendo kuliko kuandaliwa ndama aliyenona kwa chuki.
Parempi on ateria kaalia rakkaudessa, kuin syötetty härkä vihassa.
18 Mtu mwenye hasira huchochea mabishano, bali mtu ambaye hukawia kukasirika hutuliza ugomvi.
Vihainen mies saattaa toran matkaan; mutta kärsivällinen asettaa riidan.
19 Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
Laiskan tie on orjantappurainen; vaan hurskasten tie on tasainen.
20 Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
Viisas poika iloittaa isänsä, ja hullu ihminen häpäisee äitinsä.
21 Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
Hulluulle on tyhmyys iloksi; vaan toimellinen mies pysyy oikialla tiellä.
22 Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
Aivoitus raukee ilman neuvoaa; vaan jossa monta neuvonantajaa on, se on vahva.
23 Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
Se on ihmisen ilo, että hän toimella vastata taitaa, ja aikanansa sanottu sana on otollinen.
24 Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu. (Sheol )
Elämän tie johdattaa viisaan ylöspäin, välttämään helvettiä, joka alhaalla on. (Sheol )
25 Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
Herra ylpeiden huoneet kukistaa, ja vahvistaa lesken rajat.
26 Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
Ilkiäin aivoitukset ovat Herralle kauhistukseksi; vaan toimellinen puhe on otollinen.
27 Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
Ahneudella voitetut kukistavat oman huoneensa; vaan joka lahjoja vihaa, saa elää.
28 Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
Vanhurskaan sydän ajattelee vastausta; vaan jumalattoman suu ammuntaa pahaa.
29 Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
Herra on kaukana jumalattomista; vaan hän kuulee vanhurskasten rukoukset.
30 Nuru ya macho huleta furaha moyoni na habari njema ni afya kwenye mwili.
Suloinen kasvo iloittaa sydämen: hyvä sanoma tekee luut lihaviksi.
31 Kama utazingatia wakati mtu anapokurekebisha jinsi ya kuishi, utabaki miongoni mwa watu wenye busara.
Korva, joka kuulee elämän rangaistusta, on asuva viisasten seassa.
32 Yeye anayekataa karipio hujidharau mwenyewe, bali yule asikilizaye masahihisho hujipatia ufahamu.
Joka ei itsiänsä salli kurittaa, se katsoo ylön sielunsa; vaan joka rangaistusta kuulee, hän tulee viisaaksi.
33 Kumcha Yehova hufundisha hekima na unyenyekevu huja kabla ya heshima.
Herran pelko on kuritus viisauteen, ja kunnian edellä käy nöyryys.