< Mithali 15 >
1 Jawabu la upole huondoa ghadhabu, bali neno la ukatili huchochea hasira.
A soft answere brekith ire; an hard word reisith woodnesse.
2 Ulimi wa watu mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha wapumbavu humwaga upuuzi.
The tunge of wise men ourneth kunnyng; the mouth of foolis buylith out foli.
3 Macho ya Yehova yapo kila mahali, yakiwatazama juu ya waovu na wema.
In ech place the iyen of the Lord biholden good men, and yuel men.
4 Ulimi unaoponya ni mti wa uzima, bali ulimi wa udanganyifu huvunja moyo.
A plesaunt tunge is the tre of lijf; but the tunge which is vnmesurable, schal defoule the spirit.
5 Mpumbavu hudharau marudi ya baba yake, bali yeye anayejifunza kutokana na masahihisho ni mwenye hekima.
A fool scorneth the techyng of his fadir; but he that kepith blamyngis, schal be maad wisere. Moost vertu schal be in plenteuouse riytfulnesse; but the thouytis of wickid men schulen be drawun vp bi the roote.
6 Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
The hous of a iust man is moost strengthe; and disturbling is in the fruitis of a wickid man.
7 Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
The lippis of wise men schulen sowe abrood kunnyng; the herte of foolis schal be vnlijc.
8 Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.
The sacrifices of wickyd men ben abhomynable to the Lord; avowis of iust men ben plesaunt.
9 Yehova anachukia njia ya watu waovu, bali anampenda yule ambaye huandama haki.
The lijf of the vnpitouse man is abhomynacioun to the Lord; he that sueth riytfulnesse, schal be loued of the Lord.
10 Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
Yuel teching is of men forsakinge the weie of lijf; he that hatith blamyngis, schal die.
11 Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu? (Sheol )
Helle and perdicioun ben open bifor the Lord; hou myche more the hertis of sones of men. (Sheol )
12 Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
A man ful of pestilence loueth not hym that repreueth him; and he goith not to wyse men.
13 Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
A ioiful herte makith glad the face; the spirit is cast doun in the morenyng of soule.
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.
The herte of a wijs man sekith techyng; and the mouth of foolis is fed with vnkunnyng.
15 Siku zote za watu waliokandamizwa ni taabu, bali moyo wenye furaha unakaramu daima.
Alle the daies of a pore man ben yuele; a sikir soule is a contynuel feeste.
16 Bora kitu kidogo pamoja na kumcha Mungu kuliko hazina kubwa pamoja na ghasia.
Betere is a litil with the drede of the Lord, than many tresouris and vnfillable.
17 Bora mlo wenye mboga kukiwa na upendo kuliko kuandaliwa ndama aliyenona kwa chuki.
It is betere to be clepid to wortis with charite, than with hatrede to a calf maad fat.
18 Mtu mwenye hasira huchochea mabishano, bali mtu ambaye hukawia kukasirika hutuliza ugomvi.
A wrathful man reisith chidyngis; he that is pacient, swagith chidyngis reisid.
19 Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
The weie of slow men is an hegge of thornes; the weie of iust men is with out hirtyng.
20 Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
A wise sone makith glad the fadir; and a fonned man dispisith his modir.
21 Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
Foli is ioye to a fool; and a prudent man schal dresse hise steppis.
22 Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
Thouytis ben distried, where no counsel is; but where many counseleris ben, tho ben confermyd.
23 Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
A man is glad in the sentence of his mouth; and a couenable word is best.
24 Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu. (Sheol )
The path of lijf is on a lernyd man; that he bowe awei fro the laste helle. (Sheol )
25 Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
The Lord schal distrie the hows of proude men; and he schal make stidefast the coostis of a widewe.
26 Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
Iuele thouytis is abhomynacioun of the Lord; and a cleene word moost fair schal be maad stidfast of hym.
27 Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
He that sueth aueryce, disturblith his hous; but he that hatith yiftis schal lyue. Synnes ben purgid bi merci and feith; ech man bowith awei fro yuel bi the drede of the Lord.
28 Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
The soule of a iust man bithenkith obedience; the mouth of wickid men is ful of yuelis.
29 Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
The Lord is fer fro wickid men; and he schal here the preyers of iust men.
30 Nuru ya macho huleta furaha moyoni na habari njema ni afya kwenye mwili.
The liyt of iyen makith glad the soule; good fame makith fat the boonys.
31 Kama utazingatia wakati mtu anapokurekebisha jinsi ya kuishi, utabaki miongoni mwa watu wenye busara.
The eere that herith the blamyngis of lijf, schal dwelle in the myddis of wise men.
32 Yeye anayekataa karipio hujidharau mwenyewe, bali yule asikilizaye masahihisho hujipatia ufahamu.
He that castith awei chastisyng, dispisith his soule; but he that assentith to blamyngis, is pesible holdere of the herte.
33 Kumcha Yehova hufundisha hekima na unyenyekevu huja kabla ya heshima.
The drede of the Lord is teching of wisdom; and mekenesse goith bifore glorie.