< Mithali 15 >

1 Jawabu la upole huondoa ghadhabu, bali neno la ukatili huchochea hasira.
A soft answere putteth away wrath: but grieuous wordes stirre vp anger.
2 Ulimi wa watu mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha wapumbavu humwaga upuuzi.
The tongue of the wise vseth knowledge aright: but the mouth of fooles babbleth out foolishnesse.
3 Macho ya Yehova yapo kila mahali, yakiwatazama juu ya waovu na wema.
The eyes of the Lord in euery place beholde the euill and the good.
4 Ulimi unaoponya ni mti wa uzima, bali ulimi wa udanganyifu huvunja moyo.
A wholesome tongue is as a tree of life: but the frowardnes therof is the breaking of ye minde.
5 Mpumbavu hudharau marudi ya baba yake, bali yeye anayejifunza kutokana na masahihisho ni mwenye hekima.
A foole despiseth his fathers instruction: but he that regardeth correction, is prudent.
6 Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
The house of the righteous hath much treasure: but in the reuenues of the wicked is trouble.
7 Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
The lippes of the wise doe spread abroade knowledge: but ye heart of the foolish doth not so.
8 Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.
The sacrifice of the wicked is abomination to the Lord: but the prayer of the righteous is acceptable vnto him.
9 Yehova anachukia njia ya watu waovu, bali anampenda yule ambaye huandama haki.
The way of the wicked is an abomination vnto the Lord: but he loueth him that followeth righteousnes.
10 Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
Instruction is euill to him that forsaketh the way, and he that hateth correction, shall die.
11 Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu? (Sheol h7585)
Hell and destruction are before the Lord: how much more the hearts of the sonnes of men? (Sheol h7585)
12 Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
A scorner loueth not him that rebuketh him, neither will he goe vnto the wise.
13 Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
A ioyfull heart maketh a chearefull countenance: but by the sorow of the heart the minde is heauie.
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.
The heart of him that hath vnderstanding, seeketh knowledge: but the mouth of the foole is fedde with foolishnes.
15 Siku zote za watu waliokandamizwa ni taabu, bali moyo wenye furaha unakaramu daima.
All the dayes of the afflicted are euill: but a good conscience is a continuall feast.
16 Bora kitu kidogo pamoja na kumcha Mungu kuliko hazina kubwa pamoja na ghasia.
Better is a litle with the feare of the Lord, then great treasure, and trouble therewith.
17 Bora mlo wenye mboga kukiwa na upendo kuliko kuandaliwa ndama aliyenona kwa chuki.
Better is a dinner of greene herbes where loue is, then a stalled oxe and hatred therewith.
18 Mtu mwenye hasira huchochea mabishano, bali mtu ambaye hukawia kukasirika hutuliza ugomvi.
An angrie man stirreth vp strife: but hee that is slowe to wrath, appeaseth strife.
19 Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
The way of a slouthfull man is as an hedge of thornes: but the way of the righteous is plaine.
20 Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
A wise sonne reioyceth the father: but a foolish man despiseth his mother.
21 Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
Foolishnes is ioy to him that is destitute of vnderstanding: but a man of vnderstanding walketh vprightly.
22 Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
Without cousel thoughts come to nought: but in the multitude of counsellers there is stedfastnesse.
23 Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
A ioy commeth to a man by the answere of his mouth: and how good is a word in due season?
24 Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu. (Sheol h7585)
The way of life is on high to the prudent, to auoyde from hell beneath. (Sheol h7585)
25 Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
The Lord will destroye the house of the proude men: but hee will stablish the borders of the widowe.
26 Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
The thoughts of ye wicked are abomination to the Lord: but the pure haue pleasant wordes.
27 Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
He that is greedie of gaine, troubleth his owne house: but he that hateth giftes, shall liue.
28 Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
The heart of the righteous studieth to answere: but the wicked mans mouth babbleth euil thinges.
29 Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
The Lord is farre off from the wicked: but he heareth the prayer of the righteous.
30 Nuru ya macho huleta furaha moyoni na habari njema ni afya kwenye mwili.
The light of the eyes reioyceth the heart, and a good name maketh the bones fat.
31 Kama utazingatia wakati mtu anapokurekebisha jinsi ya kuishi, utabaki miongoni mwa watu wenye busara.
The eare that hearkeneth to the correction of life, shall lodge among the wise.
32 Yeye anayekataa karipio hujidharau mwenyewe, bali yule asikilizaye masahihisho hujipatia ufahamu.
Hee that refuseth instruction, despiseth his owne soule: but he that obeyeth correction, getteth vnderstanding.
33 Kumcha Yehova hufundisha hekima na unyenyekevu huja kabla ya heshima.
The feare of the Lord is the instruction of wisdome: and before honour, goeth humilitie.

< Mithali 15 >