< Mithali 15 >

1 Jawabu la upole huondoa ghadhabu, bali neno la ukatili huchochea hasira.
A mild answer breaketh wrath: but a harsh word stirreth up fury.
2 Ulimi wa watu mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha wapumbavu humwaga upuuzi.
The tongue of the wise adorneth knowledge: but the mouth of fools bubbleth out folly.
3 Macho ya Yehova yapo kila mahali, yakiwatazama juu ya waovu na wema.
The eyes of the Lord in every place behold the good and the evil.
4 Ulimi unaoponya ni mti wa uzima, bali ulimi wa udanganyifu huvunja moyo.
A peaceable tongue is a tree of life: but that which is immoderate, shall crush the spirit.
5 Mpumbavu hudharau marudi ya baba yake, bali yeye anayejifunza kutokana na masahihisho ni mwenye hekima.
A fool laugheth at the instruction of his father: but he that regardeth reproofs shall become prudent. In abundant justice there is the greatest strength: but the devices of the wicked shall be rooted out.
6 Katika nyumba ya wale watendao haki kuna hazina kubwa, bali mapato ya watu waovu huwapa taabu.
The house of the just is very much strength: and in the fruits of the wicked is trouble.
7 Midomo ya wenye hekima husambaza maarifa, bali mioyo ya wapumbavu haifanyi hivyo.
The lips of the wise shall disperse knowledge: the heart of fools shall be unlike.
8 Yehova anachukia sadaka za watu waovu, bali maombi ya watu waadilifu ndiyo furaha yake.
The victims of the wicked are abominable to the Lord: the vows of the just are acceptable.
9 Yehova anachukia njia ya watu waovu, bali anampenda yule ambaye huandama haki.
The way of the wicked is an abomination to the Lord: he that followeth justice is beloved by him.
10 Marudi ya ukatili hungojea kwa yeyote ambaye huiacha njia na yule ambaye huchukia masahihisho atakufa.
Instruction is grievous to him that forsaketh the way of life: he that hateth reproof shall die.
11 Kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele za Yehova; je si zaidi sana mioyo ya wana wa wanadamu? (Sheol h7585)
Hell and destruction are before the Lord: how much more the hearts of the children of men? (Sheol h7585)
12 Mwenye mzaha huchukia masahihisho; hatakwenda kwa wenye hekima.
A corrupt man loveth not one that reproveth him: nor will he go to the wise.
13 Moyo wenye furaha husababisha uchangamfu wa uso, bali huzuni huvunja moyo.
A glad heart maketh a cheerful countenance: but by grief of mind the spirit is cast down.
14 Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa, bali kinywa cha wapumbavu hujilisha kwenye upuuzi.
The heart of the wise seeketh instruction: and the mouth of fools feedeth on foolishness.
15 Siku zote za watu waliokandamizwa ni taabu, bali moyo wenye furaha unakaramu daima.
All the days of the poor are evil: a secure mind is like a continual feast.
16 Bora kitu kidogo pamoja na kumcha Mungu kuliko hazina kubwa pamoja na ghasia.
Better is a little with the fear of the Lord, than great treasures without content,
17 Bora mlo wenye mboga kukiwa na upendo kuliko kuandaliwa ndama aliyenona kwa chuki.
It is better to be invited to herbs with love, than to a fatted calf with hatred.
18 Mtu mwenye hasira huchochea mabishano, bali mtu ambaye hukawia kukasirika hutuliza ugomvi.
A passionate man stirreth up strifes: he that is patient appeaseth those that are stirred up.
19 Mapito ya mtu goigoi ni kama sehemu yenye uwa wa miiba, bali mapito ya mtu mwadilifu ni njia kuu iliyojengwa imara.
The way of the slothful is as a hedge of thorns; the way of the just is without offence.
20 Mwana mwenye busara huleta furaha kwa baba yake, bali mtu mpumbavu humdharau mama yake.
A wise son maketh a father joyful: but the foolish man despiseth his mother.
21 Upuuzi humfurahia mtu ambaye amepungukiwa akili, bali mwenye ufahamu hutembea katika njia nyofu.
Folly is joy to the fool: and the wise man maketh straight his steps.
22 Mipango huharibika ambapo hakuna ushauri, bali washauri wengi wanafanikiwa.
Designs are brought to nothing where there is no counsel: but where there are many counsellors, they are established.
23 Mtu anapata furaha wakati anapotoa jibu la kufaa; je ni zuri kiasi gani neno kwa wakati muafaka!
A man rejoiceth in the sentence of his mouth: and a word in due time is best.
24 Njia ya uzima huwapeleka juu watu wenye hekima, ili waondoke kutoka chini kuzimu. (Sheol h7585)
The path of life is above for the wise, that he may decline from the lowest hell. (Sheol h7585)
25 Yehova hurarua urithi wa mwenye kiburi, bali huzilinda mali za mjane.
The Lord will destroy the house of the proud: and will strengthen the borders of the widow.
26 Yehova huyachukia mawazo ya watu waovu, bali maneno ya upole ni safi.
Evil thoughts are an abomination to the Lord: and pure words most beautiful shall be confirmed by him.
27 Mporaji huleta shida kwenye familia yake, bali yeye ambaye huchukia rushwa ataishi.
He that is greedy of gain troubleth his own house: but he that hateth bribes shall live. By mercy and faith sins are purged away: and by the fear of the Lord every one declineth from evil.
28 Moyo wa yule atendaye haki hutafakari kabla ya kujibu, bali kinywa cha watu waovu humwanga ubaya wake wote.
The mind of the just studieth obedience: the mouth of the wicked over floweth with evils.
29 Yehova yupo mbali na watu waovu, bali husikia maombi ya wale watendao haki.
The Lord is far from the wicked: and he will hear the prayers of the just.
30 Nuru ya macho huleta furaha moyoni na habari njema ni afya kwenye mwili.
The light of the eyes rejoiceth the soul: a good name maketh the bones fat.
31 Kama utazingatia wakati mtu anapokurekebisha jinsi ya kuishi, utabaki miongoni mwa watu wenye busara.
The ear that heareth the reproofs of life, shall abide in the midst of the wise.
32 Yeye anayekataa karipio hujidharau mwenyewe, bali yule asikilizaye masahihisho hujipatia ufahamu.
He that rejecteth instruction, despiseth his own soul: but he that yieldeth to reproof possesseth understanding.
33 Kumcha Yehova hufundisha hekima na unyenyekevu huja kabla ya heshima.
The fear of the Lord is the lesson of wisdom: and humility goeth before glory.

< Mithali 15 >