< Mithali 14 >

1 Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
Genom visa qvinnor varder huset bygdt; men en galen bryter det neder med sina åthäfvor.
2 Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
Den som Herran fruktar, han går på rätta vägen; men den honom föraktar, han viker af hans väg.
3 Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
Dårar tala tyranniskt; men de vise bevara sin mun.
4 Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
Der icke oxar äro, der är krubban ren; men der oxen hafver nog skaffa, der är nog inkommande.
5 Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
Ett troget vittne ljuger icke; men ett falskt vittne talar dristeliga lögn.
6 Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
Bespottaren söker vishet, och finner henne intet; men dem förståndiga är vishet lätt.
7 Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
Kommer du till en dåra, der finner du icke ett förnumstigt ord.
8 Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
Det är dens klokas vishet, att han aktar uppå sin väg; men det är ens dåras galenskap, att det är alltsammans bedrägeri med honom.
9 Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
De dårar drifva deras gabberi med syndene; men de fromme hafva lust till de fromma.
10 Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
När hjertat sörjandes är, så hjelper ingen utvärtes glädje.
11 Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
De ogudaktigas hus varder förgjordt; men de frommas hydda skall grönskas.
12 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
Mångom behagar en väg väl; men på ändalyktene leder han honom till döden.
13 Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
Efter löje kommer sorg, och änden på glädjene är ångest.
14 Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
Ene lösaktiga mennisko varder gåendes såsom han handlar; men en from man skall vara öfver honom.
15 Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
En fåkunnig man tror hvart ord; men en förståndig man aktar på sin gång.
16 Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
En vis man hafver fruktan, och flyr det arga; men en dåre söker fram dristeliga.
17 Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
En otålig menniska gör galen ting; men en försigtig man hatar det.
18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
De flåkote handla ovarliga; men det är de förståndigas krona, att de varliga handla.
19 Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
De onde måste buga för de goda, och de ogudaktige uti dens rättfärdigas portom.
20 Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
En fattigan hatar ock hans näste; men de rike hafva många vänner.
21 Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
Syndaren föraktar sin nästa; men säll är den som förbarmar sig öfver den elända.
22 Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
De som med illfundighet umgå, dem skall det fela; men der som godt tänka, dem skall trohet och godhet vederfaras.
23 Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
Der man arbetar, der är nog; men der man umgår med ordom, der är fattigdom.
24 Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
Dem visom är deras rikedom en krona; men de dårars galenskap blifver galenskap.
25 Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
Ett troget vittne friar lifvet; men ett falskt vittne bedrager.
26 Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
Den som Herran fruktar, han hafver ett tryggt fäste, och hans barn varda också beskärmad.
27 Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
Herrans fruktan är lifsens källa, att man må undfly dödsens snaro.
28 Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
Der en Konung mycket folk hafver, det är hans härlighet; men der litet folk är, det gör en herra blödig.
29 Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
Den som tålig är, han är vis; men den som otålig är, han uppenbarar sin galenskap.
30 Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
Ett blidt hjerta är kroppsens lif; men afund är var i benen.
31 Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
Den som försmäder den fattiga, han lastar hans skapare; men den som förbarmar sig öfver den fattiga, han ärar Gud.
32 Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
Den ogudaktige består icke uti sine olycko; men den rättfärdige är ock i dödenom frimodig.
33 Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
Uti dens förståndigas hjerta hvilar visheten, och varder uppenbar ibland dårar.
34 Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
Rättfärdighet upphöjer ett folk; men synd är folkets förderf.
35 Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.
En klok tjenare behagar Konungenom väl; men en skamlig tjenare lider han icke.

< Mithali 14 >