< Mithali 14 >
1 Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
Mądra niewiasta buduje dom swój; ale go głupia rękami swemi rozwala.
2 Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
Kto chodzi w szczerości swojej, boi się Pana; ale przewrotny w drogach swoich gardzi nim.
3 Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
W ustach głupiego jest rózga hardości; ale wargi mądrych strzegą ich.
4 Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
Gdzie niemasz wołów, żłób jest próżny; ale siłą wołów mnoży się obfitość zboża.
5 Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
Świadek prawdziwy nie kłamie; ale świadek fałszywy mówi kłamstwo.
6 Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
Naśmiewca szuka mądrości, a nie znajduje; ale umiejętność roztropnemu jest snadna.
7 Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
Idź precz od oblicza męża głupiego, gdyż nie znajdziesz przy nim warg umiejętności.
8 Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
Mądrość ostrożnego jest rozumieć drogę swoję, ale głupstwo głupich jest zdrada.
9 Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
Każdy głupi nakrywa grzech, a między uprzejmymi mieszka przyjaźń.
10 Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
Serce każdego uznaje gorzkość duszy swojej, a do wesela jego nie przymięsza się obcy.
11 Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
Dom niezbożnych zgładzony będzie; ale przybytek cnotliwych zakwitnie.
12 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
Zda się pod czas droga być prosta człowiekowi; wszakże dokończenie jej jest drogą na śmierć.
13 Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
Także i w śmiechu boleje serce, a koniec wesela bywa smutek.
14 Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
Drogami swemi nasyci się człowiek przewrotnego serca; ale się go chroni mąż dobry.
15 Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
Prostak wierzy każdemu słowu; ale ostrożny zrozumiewa postępki swoje.
16 Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
Mądry się boi, i odstępuje od złego; ale głupi dociera, i śmiałym jest.
17 Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
Porywczy człowiek dopuszcza się głupstwa, a mąż złych myśli w nienawiści bywa.
18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
Głupstwo prostacy dziedzicznie trzymają; ale ostrożni bywają koronowani umiejętnością.
19 Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
źli się kłaniają przed dobrymi, a niepobożni stoją u drzwi sprawiedliwego.
20 Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
Ubogi bywa i u przyjaciela swego w nienawiści; ale wiele jest tych, którzy bogatego miłują.
21 Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
Bliźnim swym grzesznik pogardza; ale kto ma litość nad ubogimi, błogosławionym jest.
22 Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
Izali nie błądzą, którzy wymyślają złe? a miłosierdzie i prawda należy tym, którzy wymyślają dobre.
23 Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
W każdej pracy bywa pożytek; ale gołe słowo warg tylko do nędzy służy.
24 Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
Bogactwo mądrych jest koroną ich; ale głupstwo głupich zostaje głupstwem.
25 Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
Świadek prawdziwy wyzwala duszę; ale fałszywy kłamstwo mówi.
26 Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
Kto się boi Pana, ma ufanie mocne; a synowie jego ucieczkę mieć będą.
27 Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
Bojaźń Pańska jest źródło żywota ku uchronieniu się sideł śmierci.
28 Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
W mnóstwie ludu jest zacność królewska; ale w trosze ludu zniszczenie hetmana.
29 Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
Nierychły do gniewu jest bogaty w rozum; ale porywczy pokazuje głupstwo.
30 Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
Serce zdrowe jest żywotem ciała; ale zazdrość jest zgniłością w kościach.
31 Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
Kto ciemięży ubogiego, uwłacza stworzycielowi jego; ale go czci, kto ma litość nad ubogim.
32 Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
Dla złości swojej wygnany bywa niepobożny; ale sprawiedliwy nadzieję ma i przy śmierci swojej.
33 Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
W sercu mądrego odpoczywa mądrość, ale wnet poznać, co jest w sercu głupich.
34 Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
Sprawiedliwość wywyższa naród; ale grzech jest ku pohańbieniu narodów.
35 Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.
Król łaskaw bywa na sługę roztropnego; ale się gniewa na tego, który mu hańbę czyni.