< Mithali 14 >

1 Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
sapiens mulier aedificavit domum suam insipiens instructam quoque destruet manibus
2 Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
ambulans recto itinere et timens Deum despicitur ab eo qui infami graditur via
3 Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
in ore stulti virga superbiae labia sapientium custodiunt eos
4 Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
ubi non sunt boves praesepe vacuum est ubi autem plurimae segetes ibi manifesta fortitudo bovis
5 Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
testis fidelis non mentietur profert mendacium testis dolosus
6 Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
quaerit derisor sapientiam et non inveniet doctrina prudentium facilis
7 Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
vade contra virum stultum et nescito labia prudentiae
8 Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
sapientia callidi est intellegere viam suam et inprudentia stultorum errans
9 Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
stultis inludet peccatum inter iustos morabitur gratia
10 Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
cor quod novit amaritudinem animae suae in gaudio eius non miscebitur extraneus
11 Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
domus impiorum delebitur tabernacula iustorum germinabunt
12 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
est via quae videtur homini iusta novissima autem eius deducunt ad mortem
13 Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
risus dolore miscebitur et extrema gaudii luctus occupat
14 Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
viis suis replebitur stultus et super eum erit vir bonus
15 Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
innocens credit omni verbo astutus considerat gressus suos
16 Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
sapiens timet et declinat malum stultus transilit et confidit
17 Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
inpatiens operabitur stultitiam et vir versutus odiosus est
18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
possidebunt parvuli stultitiam et astuti expectabunt scientiam
19 Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
iacebunt mali ante bonos et impii ante portas iustorum
20 Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
etiam proximo suo pauper odiosus erit amici vero divitum multi
21 Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
qui despicit proximum suum peccat qui autem miseretur pauperi beatus erit
22 Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
errant qui operantur malum misericordia et veritas praeparant bona
23 Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
in omni opere erit abundantia ubi autem verba sunt plurima frequenter egestas
24 Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
corona sapientium divitiae eorum fatuitas stultorum inprudentia
25 Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
liberat animas testis fidelis et profert mendacia versipellis
26 Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
in timore Domini fiducia fortitudinis et filiis eius erit spes
27 Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
timor Domini fons vitae ut declinet a ruina mortis
28 Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
in multitudine populi dignitas regis et in paucitate plebis ignominia principis
29 Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
qui patiens est multa gubernatur prudentia qui autem inpatiens exaltat stultitiam suam
30 Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
vita carnium sanitas cordis putredo ossuum invidia
31 Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
qui calumniatur egentem exprobrat factori eius honorat autem eum qui miseretur pauperis
32 Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
in malitia sua expelletur impius sperat autem iustus in morte sua
33 Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
in corde prudentis requiescit sapientia et indoctos quoque erudiet
34 Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
iustitia elevat gentem miseros facit populos peccatum
35 Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.
acceptus est regi minister intellegens iracundiam eius inutilis sustinebit

< Mithali 14 >