< Mithali 14 >

1 Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
wise woman to build house: home her and folly in/on/with hand her to overthrow him
2 Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
to go: walk in/on/with uprightness his afraid LORD and be devious way: conduct his to despise him
3 Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
in/on/with lip fool(ish) branch pride and lips wise to keep: guard them
4 Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
in/on/with nothing cattle crib pure and abundance produce in/on/with strength cattle
5 Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
witness faithful not to lie and to breathe lie witness deception
6 Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
to seek to mock wisdom and nothing and knowledge to/for to understand to lighten
7 Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
to go: went from before to/for man fool and not to know lip: words knowledge
8 Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
wisdom prudent to understand way: conduct his and folly fool deceit
9 Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
fool(ish) to mock guilt (offering) and between upright acceptance
10 Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
heart to know bitterness soul: myself his and in/on/with joy his not to pledge be a stranger
11 Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
house: household wicked to destroy and tent upright to sprout
12 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
there way: conduct upright to/for face of man and end her way: conduct death
13 Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
also in/on/with laughter to pain heart and end her joy grief
14 Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
from way: conduct his to satisfy to turn heart and from upon him man pleasant
15 Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
simple be faithful to/for all word: thing and prudent to understand to/for step his
16 Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
wise afraid and to turn aside: depart from bad: evil and fool be arrogant and to trust
17 Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
short face: anger to make: do folly and man plot to hate
18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
to inherit simple folly and prudent to surround knowledge
19 Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
to bow bad: evil to/for face: before pleasant and wicked upon gate righteous
20 Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
also to/for neighbor his to hate be poor and to love: friend rich many
21 Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
to despise to/for neighbor his to sin and be gracious (poor *Q(K)*) blessed he
22 Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
not to go astray to plow/plot bad: evil and kindness and truth: faithful to plow/plot good
23 Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
in/on/with all toil to be advantage and word: because lip: words surely to/for need
24 Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
crown wise riches their folly fool folly
25 Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
to rescue soul: life witness truth: true and to breathe lie deceit
26 Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
in/on/with fear LORD confidence strength and to/for son: child his to be refuge
27 Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
fear LORD fountain life to/for to turn aside: depart from snare death
28 Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
in/on/with abundance people adornment king and in/on/with end people terror prince
29 Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
slow face: anger many understanding and short spirit: temper to exalt folly
30 Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
life flesh heart healing and rottenness bone jealousy
31 Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
to oppress poor to taunt to make him and to honor: honour him be gracious needy
32 Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
in/on/with distress: evil his to thrust wicked and to seek refuge in/on/with death his righteous
33 Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
in/on/with heart to understand to rest wisdom and in/on/with entrails: among fool to know
34 Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
righteousness to exalt nation and shame people sin
35 Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.
acceptance king to/for servant/slave be prudent and fury his to be be ashamed

< Mithali 14 >