< Mithali 14 >

1 Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
Every wise woman has built her house, And the foolish breaks it down with her hands.
2 Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
Whoever is walking in his uprightness is fearing YHWH, And the perverted is despising Him [in] his ways.
3 Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
A rod of pride [is] in the mouth of a fool, And the lips of the wise preserve them.
4 Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
Without oxen a stall [is] clean, And great [is] the increase by the power of the ox.
5 Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
A faithful witness does not lie, And a false witness breathes out lies.
6 Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
A scorner has sought wisdom, and it is not, And knowledge [is] easy to the intelligent.
7 Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
Go from before a foolish man, Or you have not known the lips of knowledge.
8 Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
The wisdom of the prudent [is] to understand his way, And the folly of fools [is] deceit.
9 Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
Fools mock at a guilt-offering, And among the upright—a pleasing thing.
10 Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
The heart knows its own bitterness, And a stranger does not interfere with its joy.
11 Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
The house of the wicked is destroyed, And the tent of the upright flourishes.
12 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
There is a way—right before a man, And its latter end [are] ways of death.
13 Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
Even in laughter is the heart pained, And the latter end of joy [is] affliction.
14 Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
The backslider in heart is filled from his ways, And a good man—from his fruits.
15 Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
The simple gives credence to everything, And the prudent attends to his step.
16 Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
The wise is fearing and turning from evil, And a fool is transgressing and is confident.
17 Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
Whoever is short of temper does folly, And a man of wicked schemes is hated.
18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
The simple have inherited folly, And the prudent are crowned [with] knowledge.
19 Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
The evil have bowed down before the good, And the wicked at the gates of the righteous.
20 Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
The poor is hated even of his neighbor, And those loving the rich [are] many.
21 Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
Whoever is despising his neighbor sins, Whoever is favoring the humble, O his blessedness.
22 Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
Do they who are devising evil not err? And kindness and truth [are] to those devising good,
23 Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
In all labor there is advantage, And a thing of the lips [is] only to want.
24 Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
The crown of the wise is their wealth, The folly of fools [is] folly.
25 Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
A true witness is delivering souls, And a deceitful one breathes out lies.
26 Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
Strong confidence [is] in the fear of YHWH, And there is a refuge to His sons.
27 Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
The fear of YHWH [is] a fountain of life, To turn aside from snares of death.
28 Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
The honor of a king [is] in the multitude of a people, And the ruin of a prince in lack of people.
29 Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
Whoever is slow to anger [is] of great understanding, And whoever is short in temper is exalting folly.
30 Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
A healed heart [is] life to the flesh, And rottenness to the bones [is] envy.
31 Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
An oppressor of the poor reproaches his Maker, And whoever is honoring Him Is favoring the needy.
32 Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
The wicked is driven away in his wickedness, And the righteous [is] trustful in his death.
33 Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
Wisdom rests in the heart of the intelligent. And it is known in the midst of fools.
34 Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
Righteousness exalts a nation, And the righteousness of peoples [is] a sin-offering.
35 Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.
The favor of a king [is] to a wise servant, And one causing shame is an object of his wrath!

< Mithali 14 >