< Mithali 14 >
1 Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
Every wise woman builds her house, but the stupid woman tears it down with her own hands.
2 Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
Those who live right respect the Lord, but those who live dishonestly despise him.
3 Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
What stupid people say punishes their pride, but what wise people say will protect them.
4 Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
Without oxen, the manger is empty, but a good harvest comes through the ox's strength.
5 Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
A trustworthy witness doesn't lie, but a false witness is deceptive.
6 Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
It's pointless for a scoffer to look for wisdom, but knowledge comes easily to someone who understands.
7 Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
Stay away from stupid people—you won't learn anything from them.
8 Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
Sensible people use their wisdom to decide where they're going, but the foolishness of stupid people is treacherous.
9 Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
Stupid people laugh at sin, but good people want forgiveness.
10 Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
The individual's mind alone knows its sadnesses, and no one else can share its happiness.
11 Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
The house of wicked people will be destroyed, but the tent of good people will prosper.
12 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
There's a way that seems to be right, but in the end it's the way of death.
13 Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
Even when you're laughing you can be feeling sad—joy can end in grief.
14 Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
Disloyal people are repaid for what they do, and good people are rewarded.
15 Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
Stupid people believe whatever they're told, but sensible people think about what they're doing.
16 Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
Wise people are careful and avoid evil, but stupid people are confidently reckless.
17 Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
Quick-tempered people act foolishly, while people who make evil plans are hated.
18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
The inheritance of stupid people is stupidity, but sensible people are rewarded with knowledge.
19 Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
Evil people bow down before good people, and the wicked bow down at the doors of those who do right.
20 Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
The poor are hated even by their neighbors, while the rich have many friends.
21 Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
People who look down on their neighbors are sinners, but those who are kind to the poor are blessed.
22 Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
Aren't people who plan to do evil wrong? But those who plan to do good have trustworthy love and faithfulness.
23 Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
There's profit in hard work, but chatting just leads to poverty.
24 Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
The wise are rewarded with wealth, but stupid people are rewarded with stupidity.
25 Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
A truthful witness saves lives, but a false witness is treacherous.
26 Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
People who honor the Lord are completely safe; he will protect their children.
27 Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
Respecting the Lord is like a fountain of life, so you can avoid the snares of death.
28 Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
The glory of a king is the number of his subjects, for a ruler is nothing without them.
29 Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
If you're slow to get angry, you're very wise; but if you have a short fuse you glorify stupidity.
30 Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
A peaceful mind makes your body healthy, but jealousy makes your bones rot.
31 Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
Anyone who oppresses the poor insults their Maker, but anyone who is kind to the needy honors him.
32 Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
Wicked people are brought down by their own evil actions, but those who live right are confident even in death.
33 Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
Wisdom is at home in a mind that understands, but it's not found among stupid people.
34 Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
Doing right makes a nation successful, but sin is a disgrace to any people.
35 Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.
A servant who acts wisely is appreciated by the king, but he gets angry with a servant who acts disgracefully.