< Mithali 14 >

1 Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
Every wise woman builds her house, but a foolish one tears it down with her own hands.
2 Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
He who walks in uprightness fears the LORD, but the one who is devious in his ways despises Him.
3 Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
The proud speech of a fool brings a rod to his back, but the lips of the wise protect them.
4 Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
Where there are no oxen, the manger is empty, but an abundant harvest comes through the strength of the ox.
5 Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
An honest witness does not deceive, but a dishonest witness pours forth lies.
6 Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
A mocker seeks wisdom and finds none, but knowledge comes easily to the discerning.
7 Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
Stay away from a foolish man; you will gain no knowledge from his speech.
8 Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
The wisdom of the prudent is to discern his way, but the folly of fools deceives them.
9 Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
Fools mock the making of amends, but goodwill is found among the upright.
10 Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
The heart knows its own bitterness, and no stranger shares in its joy.
11 Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
The house of the wicked will be destroyed, but the tent of the upright will flourish.
12 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
There is a way that seems right to a man, but its end is the way of death.
13 Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
Even in laughter the heart may ache, and joy may end in sorrow.
14 Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
The backslider in heart receives the fill of his own ways, but a good man is rewarded for his ways.
15 Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
The simple man believes every word, but the prudent man watches his steps.
16 Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
A wise man fears and turns from evil, but a fool is careless and reckless.
17 Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
A quick-tempered man acts foolishly, and a devious man is hated.
18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
The simple inherit folly, but the prudent are crowned with knowledge.
19 Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
The evil bow before the good, and the wicked at the gates of the righteous.
20 Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
The poor man is hated even by his neighbor, but many are those who love the rich.
21 Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
He who despises his neighbor sins, but blessed is he who shows kindness to the poor.
22 Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
Do not those who contrive evil go astray? But those who plan goodness find loving devotion and faithfulness.
23 Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
There is profit in all labor, but mere talk leads only to poverty.
24 Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
The crown of the wise is their wealth, but the effort of fools is folly.
25 Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
A truthful witness saves lives, but one who utters lies is deceitful.
26 Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
He who fears the LORD is secure in confidence, and his children shall have a place of refuge.
27 Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
The fear of the LORD is a fountain of life, turning a man from the snares of death.
28 Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
A large population is a king’s splendor, but a lack of subjects is a prince’s ruin.
29 Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
A patient man has great understanding, but a quick-tempered man promotes folly.
30 Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
A tranquil heart is life to the body, but envy rots the bones.
31 Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
Whoever oppresses the poor taunts their Maker, but whoever is kind to the needy honors Him.
32 Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
The wicked man is thrown down by his own sin, but the righteous man has a refuge even in death.
33 Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
Wisdom rests in the heart of the discerning; even among fools she is known.
34 Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
Righteousness exalts a nation, but sin is a disgrace to any people.
35 Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.
A king delights in a wise servant, but his anger falls on the shameful.

< Mithali 14 >