< Mithali 14 >
1 Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
Ženska mudrost sagradi kuću, a ludost je rukama razgrađuje.
2 Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
Tko živi s poštenjem, boji se Jahve, a tko ide stranputicom, prezire ga.
3 Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
U luđakovim je ustima šiba za oholost njegovu, a mudre štite vlastite usne.
4 Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
Gdje nema volova, prazne su jasle, a obilna je žetva od snage bikove.
5 Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
Istinit svjedok ne laže, a krivi svjedok širi laž.
6 Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
Podsmjevač traži mudrost i ne nalazi je, a razumni lako dolazi do znanja.
7 Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
Idi od čovjeka bezumna jer nećeš upoznati usne što zbore znanje.
8 Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
Mudrost je pametna čovjeka u tom što pazi na svoj put, a bezumnička ludost prijevara je.
9 Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
Luđacima je grijeh šala, a milost je Božja s poštenima.
10 Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
Srce poznaje svoj jad, i veselje njegovo ne može dijeliti nitko drugi.
11 Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
Dom opakih propast će, a šator će pravednika procvasti.
12 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
Neki se put učini čovjeku prav, a na koncu vodi k smrti.
13 Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
I u smijehu srce osjeća bol, a poslije veselja dolazi tuga.
14 Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
Otpadnik se siti svojim prestupcima, a dobar čovjek svojim radom.
15 Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
Glupan vjeruje svakoj riječi, a pametan pazi na korak svoj.
16 Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
Mudar se boji i oda zla se uklanja, a bezuman se raspaljuje i bez straha je.
17 Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
Nagao čovjek čini ludosti, a razborit ih podnosi.
18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
Glupaci baštine ludost, a mudre ovjenčava znanje.
19 Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
Zli padaju ničice pred dobrima i opaki pred vratima pravednikovim.
20 Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
I svom prijatelju mrzak je siromah, a bogataš ima mnogo ljubitelja.
21 Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
Griješi tko prezire bližnjega svoga, a blago onomu tko je milostiv ubogima.
22 Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
Koji snuju zlo, ne hode li stranputicom, a zar nisu dobrota i vjernost s onima koji snuju dobro?
23 Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
U svakom trudu ima probitka, a pusto brbljanje samo je na siromaštvo.
24 Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
Mudrima je vijenac bogatstvo njihovo, a bezumnima kruna - njihova ludost.
25 Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
Istinit svjedok izbavlja duše, a tko laži širi, taj je varalica.
26 Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
U strahu je Gospodnjem veliko pouzdanje i njegovim je sinovima utočište.
27 Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
Strah Gospodnji izvor je života: on izbavlja od zamke smrti.
28 Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
Mnoštvo je naroda ponos kralju, a bez puka knez propada.
29 Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
Tko se teško srdi, velike je razboritosti, a nabusit duhom pokazuje ludost.
30 Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
Mirno je srce život tijelu, a ljubomor je gnjilež u kostima.
31 Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
Tko tlači siromaha huli na stvoritelja, a časti ga tko je milostiv ubogomu.
32 Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
Opaki propada zbog vlastite pakosti, a pravednik i u samoj smrti nalazi utočište.
33 Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
U razumnu srcu mudrost počiva, a što je u bezumnome, to se i pokaže.
34 Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
Pravednost uzvisuje narod, a grijeh je sramota pucima.
35 Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.
Kralju je mio razborit sluga, a na sramotna se srdi.