< Mithali 13 >
1 Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
O filho sábio [ouve] a correção do pai; mas o zombador não escuta a repreensão.
2 Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
Cada um comerá do bem pelo fruto de sua boca, mas a alma dos infiéis [deseja] a violência.
3 Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
Quem toma cuidado com sua boca preserva sua alma; mas aquele que abre muito seus lábios será arruinado.
4 Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
A alma do preguiçoso deseja, mas nada [consegue]; porém a alma dos trabalham com empenho prosperará.
5 Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
O justo odeia a palavra mentirosa, mas o perverso age de forma repugnante e vergonhosa.
6 Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
A justiça guarda aquele que tem um caminho íntegro; mas a perversidade transtornará ao pecador.
7 Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
Há [alguns] que fingem ser ricos, mesmo nada tendo; e [outros] que fingem ser pobres, mesmo tendo muitos bens.
8 Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
O resgate da vida de cada um são suas riquezas; mas o pobre não ouve ameaças.
9 Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
A luz dos justos se alegra, mas a lâmpada dos perversos se apagará.
10 Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
A arrogância só produz brigas; mas com os que aceitam conselhos [está] a sabedoria.
11 Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
A riqueza [ganha] sem esforço será perdida; mas aquele que a obtém pelas próprias mãos terá cada vez mais.
12 Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
A esperança que demora enfraquece o coração, mas o desejo cumprido é [como] uma árvore de vida.
13 Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
Quem despreza a [boa] palavra perecerá; mas aquele que teme ao mandamento será recompensado.
14 Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
A doutrina do sábio é manancial de vida, para se desviar das ciladas da morte.
15 Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
O bom entendimento alcança o favor, mas o caminho dos infiéis é áspero.
16 Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
Todo prudente age com conhecimento, mas o tolo espalha sua loucura.
17 Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
O mensageiro perverso cai no mal, mas o representante fiel é [como] um remédio.
18 Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
[Haverá] pobreza e vergonha ao que rejeita a correção; mas aquele que atende à repreensão será honrado.
19 Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
O desejo realizado agrada a alma, mas os tolos abominam se afastar do mal.
20 Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
Quem anda com os sábios se torna sábio; mas aquele que acompanha os tolos sofrerá.
21 Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
O mal perseguirá os pecadores, mas os justos serão recompensados com o bem.
22 Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
O homem de bem deixará herança aos filhos de seus filhos; mas a riqueza do pecador está reservada para o justo.
23 Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
A lavoura dos pobres [gera] muita comida; mas há [alguns] que se destroem por falta de juízo.
24 Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
Aquele que retém sua vara odeia a seu filho; porém aquele que o ama, desde cedo o castiga.
25 Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.
O justo come até sua alma estar saciada; mas o ventre dos perversos passará por necessidade.