< Mithali 13 >
1 Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
Den vise son let seg aga av far sin, men spottaren høyrer ikkje på skjenn.
2 Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
Sjølv fær ein godt av den frukt som munnen ber, men hugen åt svikarar stend etter vald.
3 Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
Den som agtar munnen sin, varar si sjæl, men gapen fær seg ei ulukka.
4 Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
Hugen i letingen lyster og fær ikkje noko, hugen i strævsame folk fær rikleg mette.
5 Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
Den rettferdige hatar ljugarord, men den gudlause fer stygt og skamleg åt.
6 Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
Rettferd varar den som fer ulastande, men gudløysa feller den som gjer synd.
7 Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
Mang ein ter seg rik og eig då inkje, ein annan ter seg fatig og eig mykje.
8 Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
Mannsens rikdom er ein løysepeng for livet hans, men fatigmannen fær inkje trugsmål høyra.
9 Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
Ljoset åt dei rettferdige brenn lystigt, men lampa åt ugudlege vil slokna.
10 Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
Med ovmod veld ein berre trætta, men hjå deim som tek mot råd, er visdom.
11 Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
Lettfengen rikdom minkar, men sankar du smått um senn, fær du meir og meir.
12 Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
Langdrøg von gjer hjarta sjukt, men uppfyllt ynskje er eit livsens tre.
13 Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
Den som vanvyrder ordet, tyner seg sjølv, men den som ottast bodordet, fær løn.
14 Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
Vismanns læra er livsens kjelda, so ein slepp undan frå daudesnaror.
15 Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
Godt vit gjev manntekkje, men hard er vegen som svikarar gjeng.
16 Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
Kvar som er klok, fer fram med vit, men ein dåre briskar seg med dårskap.
17 Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
Ein gudlaus sendemann fell i ulukka, men trufast bodberar er lækjedom.
18 Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
Armod og skam fær den som viser age ifrå seg, men den som agtar på refsing, vinn æra.
19 Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
Uppfyllt ynskje er søtt for sjæli, men å vika frå vondt er ei gruv for dårar.
20 Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
Gakk saman med dei vise, so vert du vis, men ilag med dårar gjeng det deg ille.
21 Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
Ulukka forfylgjer syndarar, men rettferdige fær godt til løn.
22 Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
Den gode let etter seg arv til barneborn, men det syndaren eig, er gøymt åt den rettferdige.
23 Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
Fatigfolks nybrot gjev rikeleg føda, men mang ein vert tynt ved urettferd.
24 Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
Den som sparer riset sitt, hatar son sin, men den som elskar han, tuktar honom tidleg.
25 Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.
Rettferdige hev mat til å metta seg på, men gudlause gjeng med magen tom.