< Mithali 13 >
1 Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
A wise son listeneth to the instruction of his father; But a scoffer listeneth not to rebuke.
2 Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
By the fruit of a man's mouth he shall eat good; But the appetite of transgressors shall be sated with violence.
3 Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
He who keepeth his mouth keepeth his life; But destruction shall be to him who openeth wide his lips.
4 Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
The appetite of the sluggard longeth, and hath nothing; But the appetite of the diligent is fully satisfied.
5 Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
A righteous man hateth words of falsehood; But a wicked man causeth disgrace and shame.
6 Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
Righteousness preserveth him who is upright in his way; But wickedness overthroweth the sinner.
7 Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
There is who maketh himself rich, yet hath nothing, Who maketh himself poor, yet hath great riches.
8 Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
A man's wealth is the ransom of his life; But the poor man heareth no threatenings.
9 Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
The light of the righteous shall rejoice; But the lamp of the wicked shall be put out.
10 Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
By pride cometh only contention; But with the well-advised is wisdom.
11 Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
Wealth gotten by vanity will become small; But he who gathereth it into the hand increaseth it.
12 Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
Hope deferred maketh the heart sick; But the desire accomplished is a tree of life.
13 Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
He that despiseth the word shall be destroyed; But he who revereth the commandment shall be rewarded.
14 Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
The instruction of the wise is a fountain of life; By it men escape from the snares of death.
15 Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
A good understanding winneth favor; But the way of transgressors is hard.
16 Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
Every prudent man acteth with knowledge; But a fool spreadeth abroad his folly.
17 Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
A wicked messenger falleth into trouble; But a faithful ambassador is health.
18 Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
Poverty and shame are for him who rejecteth instruction; But he that regardeth reproof shall come to honor.
19 Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
The desire accomplished is sweet to the soul; But it is an abomination to fools to depart from evil.
20 Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
He who walketh with wise men shall be wise; But the companion of fools shall be destroyed.
21 Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
Calamity pursueth the wicked; But the righteous is rewarded with good.
22 Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
The good man leaveth his substance to his children's children; But the wealth of the sinner is laid up for the just.
23 Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
There is much food from the fallow-ground of the poor; But there is who is brought low for want of uprightness.
24 Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
He that spareth the rod hateth his son; But he who loveth him chasteneth him early.
25 Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.
The righteous man eateth to the satisfying of his desire; But the stomach of the wicked suffereth want.