< Mithali 13 >

1 Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
A wise son is instructed of his father; but a scorner heareth not rebuke.
2 Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
A man shall eat good from the fruit of his mouth; but the desire of the faithless is violence.
3 Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
He that guardeth his mouth keepeth his life; but for him that openeth wide his lips there shall be ruin.
4 Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
The soul of the sluggard desireth, and hath nothing; but the soul of the diligent shall be abundantly gratified.
5 Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
A righteous man hateth lying; but a wicked man behaveth vilely and shamefully.
6 Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
Righteousness guardeth him that is upright in the way; but wickedness overthroweth the sinner.
7 Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
There is that pretendeth himself rich, yet hath nothing; there is that pretendeth himself poor, yet hath great wealth.
8 Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
The ransom of a man's life are his riches; but the poor heareth no threatening.
9 Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
The light of the righteous rejoiceth; but the lamp of the wicked shall be put out.
10 Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
By pride cometh only contention; but with the well-advised is wisdom.
11 Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
Wealth gotten by vanity shall be diminished; but he that gathereth little by little shall increase.
12 Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
Hope deferred maketh the heart sick; but desire fulfilled is a tree of life.
13 Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
Whoso despiseth the word shall suffer thereby; but he that feareth the commandment shall be rewarded.
14 Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
The teaching of the wise is a fountain of life, to depart from the snares of death.
15 Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
Good understanding giveth grace; but the way of the faithless is harsh.
16 Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
Every prudent man dealeth with forethought; but a fool unfoldeth folly.
17 Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
A wicked messenger falleth into evil; but a faithful ambassador is health.
18 Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
Poverty and shame shall be to him that refuseth instruction; but he that regardeth reproof shall be honoured.
19 Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
The desire accomplished is sweet to the soul; and it is an abomination to fools to depart from evil.
20 Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
He that walketh with wise men shall be wise; but the companion of fools shall smart for it.
21 Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
Evil pursueth sinners; but to the righteous good shall be repaid.
22 Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
A good man leaveth an inheritance to his children's children; and the wealth of the sinner is laid up for the righteous.
23 Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
Much food is in the tillage of the poor; but there is that is swept away by want of righteousness.
24 Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
He that spareth his rod hateth his son; but he that loveth him chasteneth him betimes.
25 Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.
The righteous eateth to the satisfying of his desire; but the belly of the wicked shall want.

< Mithali 13 >