< Mithali 13 >
1 Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
A wise sonne will obey the instruction of his father: but a scorner will heare no rebuke.
2 Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
A man shall eate good things by the fruite of his mouth: but the soule of the trespassers shall suffer violence.
3 Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
Hee that keepeth his mouth, keepeth his life: but he that openeth his lips, destruction shall be to him.
4 Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
The sluggard lusteth, but his soule hath nought: but the soule of the diligent shall haue plentie.
5 Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
A righteous man hateth lying wordes: but the wicked causeth slander and shame.
6 Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
Righteousnesse preserueth the vpright of life: but wickednes ouerthroweth the sinner.
7 Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
There is that maketh himselfe riche, and hath nothing, and that maketh himselfe poore, hauing great riches.
8 Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
A man will giue his riches for the ransome of his life: but the poore cannot heare ye reproch.
9 Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
The light of the righteous reioyceth: but the candle of the wicked shall be put out.
10 Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
Onely by pride doeth man make contention: but with the well aduised is wisdome.
11 Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
The riches of vanitie shall diminish: but he that gathereth with the hand, shall increase them.
12 Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
The hope that is deferred, is the fainting of the heart: but when the desire commeth, it is as a tree of life.
13 Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
He that despiseth the worde, hee shall be destroyed: but hee that feareth the commandement he shalbe rewarded.
14 Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
The instruction of a wise man is as the welspring of life, to turne away from the snares of death.
15 Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
Good vnderstanding maketh acceptable: but the way of the disobedient is hated.
16 Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
Euery wise man will worke by knowledge: but a foole will spread abroade folly.
17 Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
A wicked messenger falleth into euill: but a faithfull ambassadour is preseruation.
18 Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
Pouertie and shame is to him that refuseth instruction: but hee that regardeth correction, shalbe honoured.
19 Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
A desire accomplished deliteth ye soule: but it is an abomination to fooles to depart from euil.
20 Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
He that walketh with the wise, shalbe wise: but a companion of fooles shalbe afflicted.
21 Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
Affliction followeth sinners: but vnto the righteous God will recompense good.
22 Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
The good man shall giue inheritance vnto his childrens children: and the riches of the sinner is layde vp for the iust.
23 Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
Much foode is in the fielde of the poore: but the fielde is destroyed without discretion.
24 Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
He that spareth his rodde, hateth his sonne: but he that loueth him, chasteneth him betime.
25 Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.
The righteous eateth to the contentation of his minde: but the belly of the wicked shall want.