< Mithali 12 >

1 Anayependa mafundisho hupenda maarifa, bali yule anayechukia maonyo ni mpumbavu.
to love: lover discipline to love: lover knowledge and to hate argument stupid
2 Yehova humpa fadhila mtu mwema, bali mtu ambaye hufanya mipango ya ufisada atahukumiwa.
pleasant to promote acceptance from LORD and man plot be wicked
3 Mtu hawezi kuimarishwa kwa uovu, bali wale watendao haki hawawezi kung'olewa.
not to establish: establish man in/on/with wickedness and root righteous not to shake
4 Mke mwema ni taji ya mume wake, bali yule aletaye aibu ni kama ugonjwa unaoozesha mifupa yake.
woman: wife strength: worthy crown master: husband her and like/as rottenness in/on/with bone his be ashamed
5 Mipango ya wale watendao haki ni adili, bali shauri la mwovu ni udanganyifu.
plot righteous justice counsel wicked deceit
6 Maneno ya watu waovu ni uviziaji unaosubiri nafasi ya kuua, bali maneno ya mwenye haki yatawatunza salama.
word wicked to ambush blood and lip upright to rescue them
7 Watu waovu wametupwa na kuondolewa, bali nyumba ya wale watendao haki itasimama.
to overturn wicked and nothing they and house: home righteous to stand: stand
8 Mtu husifiwa kwa kadri ya hekima yake, bali yule anayechagua ukaidi hudharauliwa.
to/for lip: according understanding his to boast: praise man and to twist heart to be to/for contempt
9 Bora kuwa na cheo duni- kuwa mtumishi tu- kuliko kujisifu kuhusu ukuu wako bila kuwa na chakula.
pleasant to dishonor and servant/slave to/for him from to honor: honour and lacking food: bread
10 Yule atendaye haki anajali mahitaji ya mnyama wake, bali huruma ya mwovu ni ukatili.
to know righteous soul: life animal his and compassion wicked cruel
11 Yule atendaye kazi katika shamba lake atapata chakula tele, bali anayesaka miradi duni hana akili.
to serve: labour land: soil his to satisfy food: bread and to pursue worthless lacking heart
12 Watu waovu hutamani wanavyoiba watu wabaya kutoka kwa wengine, bali tunda la wale watendao haki hutoka kwao mwenyewe.
to desire wicked net bad: evil and root righteous to give: give
13 Mtu mbaya hunaswa kwa maongezi yake mabaya, bali wale watendao haki hujinasua katika taabu.
in/on/with transgression lips snare bad: evil and to come out: come from distress righteous
14 Mtu hushiba vitu vyema kutokana na tunda la maneno yake, kama vile kazi ya mikono yake inavyompa thawabu.
from fruit lip man to satisfy good and recompense hand man (to return: return *Q(K)*) to/for him
15 Njia ya mpumbavu ni sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu wa hekima husikiliza ushauri.
way: conduct fool(ish) upright in/on/with eye his and to hear: hear to/for counsel wise
16 Mpumbavu huonyesha hasira yake papo hapo, bali asiyejali tusi ni mwenye busara.
fool(ish) in/on/with day: today to know vexation his and to cover dishonor prudent
17 Asemaye ukweli huongea ilivyo haki, bali shahidi wa uongo huongea uongo.
to breathe faithfulness to tell righteousness and witness deception deceit
18 Maneno yake asemaye kwa pupa ni kama kurusha upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
there to speak rashly like/as thrust sword and tongue wise healing
19 Midomo yenye kweli itadumu milele, bali ulimi wa uongo ni kwa kitambo kidogo tu.
lips truth: true to establish: establish to/for perpetuity and till to disturb tongue deception
20 Kuna udanganyifu katika mioyo ya wale wanaopanga kutenda uovu, bali furaha hutoka kwa washauri wa amani.
deceit in/on/with heart to plow/plot bad: evil and to/for to advise peace joy
21 Hakuna ugonjwa utakaowajia wale watendao haki, bali watu waovu watajazwa matatizo.
not to meet to/for righteous all evil: trouble and wicked to fill bad: evil
22 Yehova anachukia midomo ya uongo, bali wale ambao huishi kwa uaminifu ndiyo furaha yake.
abomination LORD lips deception and to make: do faithfulness acceptance his
23 Mtu mwenye busara anasitiri maarifa yake, bali moyo wa wapumbavu hupiga yowe za kipumbavu.
man prudent to cover knowledge and heart fool to call: call out folly
24 Mkono wa mwenye bidii utatawala, bali watu wavivu watawekwa katika kazi za kulazimishwa.
hand sharp to rule (and slackness *L(bah)*) to be to/for taskworker
25 Mashaka katika moyo wa mtu humwelemea, bali neno zuri humfurahisha.
anxiety in/on/with heart man to bow her and word pleasant to rejoice her
26 Mwenye haki ni kiongozi kwa rafiki yake, bali njia ya waovu huwaongoza katika kupotea.
to spy from neighbor his righteous and way: conduct wicked to go astray them
27 Watu wavivu hawawezi kubanika mawindo yao wenyewe, bali mtu wenye bidii atapata mali zenye thamani.
not to roast slackness wild game his and substance man precious sharp
28 Wale ambao wanatembea katika njia ya haki wanapata uzima na katika mapito hayo hakuna kifo.
in/on/with way righteousness life and way: road path not death

< Mithali 12 >