< Mithali 10 >
1 Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
Provérbios de Salomão: O filho sábio alegra ao pai; mas o filho tolo é tristeza para sua mãe.
2 Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
Tesouros da perversidade para nada aproveitam; porém a justiça livra da morte.
3 Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
O SENHOR não permite a alma do justo passar fome, porém arruína o interesse dos perversos.
4 Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
Aquele que trabalha com mão preguiçosa empobrece; mas a mão de quem trabalha com empenho enriquece.
5 Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
Aquele que ajunta no verão é filho prudente; [mas] o que dorme na ceifa é filho causador de vergonha.
6 Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
Há bênçãos sobre a cabeça dos justos; mas a violência cobre a boca dos perversos.
7 Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
A lembrança do justo [será] uma bênção; mas o nome dos perversos apodrecerá.
8 Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
O sábio de coração aceita os mandamentos; mas o louco de lábios será derrubado.
9 Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
Aquele que anda em sinceridade anda seguro; mas o que perverte seus caminhos será conhecido.
10 Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
Aquele que pisca os olhos maliciosamente gera dores; e o louco de lábios será derrubado.
11 Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
A boca do justo é um manancial de vida; mas a boca dos perversos está coberta de violência.
12 Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
O ódio desperta brigas; mas o amor cobre todas as transgressões.
13 Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
Nos lábios do bom entendedor se acha sabedoria, mas uma vara está às costas daquele que não tem entendimento.
14 Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
Os sábios guardam consigo sabedoria; mas a boca do tolo [está] perto da perturbação.
15 Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
A prosperidade do rico é a sua cidade fortificada; a pobreza dos necessitados é sua perturbação.
16 Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
A obra do justo é para a vida; os frutos do perverso, para o pecado.
17 Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
O caminho para a vida [é d] aquele que guarda a correção; mas aquele que abandona a repreensão anda sem rumo.
18 Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
Aquele que esconde o ódio [tem] lábios mentirosos; e o que produz má fama é tolo.
19 Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
Na abundância de palavras não há falta de transgressão; mas aquele que refreia seus lábios é prudente.
20 Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
A língua do justo [é como] prata escolhida; o coração dos perversos [vale] pouco.
21 Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
Os lábios dos justo apascentam a muitos; mas os tolos, por falta de entendimento, morrem.
22 Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
É a bênção do SENHOR que enriquece; e ele não lhe acrescenta dores.
23 Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
Para o tolo, fazer o mal é uma diversão; mas para o homem bom entendedor, [divertida é] a sabedoria.
24 Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
O temor do perverso virá sobre ele, mas o desejo dos justos será concedido.
25 Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
Assim como o vento passa, assim também o perverso não [mais] existirá; mas o justo [tem] um alicerce eterno.
26 Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Assim como vinagre para os dentes, e como fumaça para os olhos, assim também é o preguiçoso para aqueles que o mandam.
27 Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
O temor ao SENHOR faz aumentar os dias; mas os anos dos perversos serão encurtados.
28 Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
A esperança dos justos [é] alegria; mas a expectativa dos perversos perecerá.
29 Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
O caminho do SENHOR é fortaleza para os corretos, mas ruína para os que praticam maldade.
30 Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
O justo nunca será removido, mas os perversos não habitarão a terra.
31 Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
A boca do justo produz sabedoria, mas a língua perversa será cortada fora.
32 Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.
Os lábios do justo sabem o que é agradável; mas a boca dos perversos [é cheia] de perversidades.