< Mithali 10 >

1 Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
parabolae Salomonis filius sapiens laetificat patrem filius vero stultus maestitia est matris suae
2 Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
non proderunt thesauri impietatis iustitia vero liberabit a morte
3 Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
non adfliget Dominus fame animam iusti et insidias impiorum subvertet
4 Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
egestatem operata est manus remissa manus autem fortium divitias parat
5 Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
qui congregat in messe filius sapiens est qui autem stertit aestate filius confusionis
6 Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
benedictio super caput iusti os autem impiorum operit iniquitatem
7 Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
memoria iusti cum laudibus et nomen impiorum putrescet
8 Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
sapiens corde praecepta suscipiet stultus caeditur labiis
9 Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
qui ambulat simpliciter ambulat confidenter qui autem depravat vias suas manifestus erit
10 Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
qui annuit oculo dabit dolorem stultus labiis verberabitur
11 Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
vena vitae os iusti et os impiorum operiet iniquitatem
12 Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
odium suscitat rixas et universa delicta operit caritas
13 Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
in labiis sapientis invenietur sapientia et virga in dorso eius qui indiget corde
14 Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
sapientes abscondunt scientiam os autem stulti confusioni proximum est
15 Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
substantia divitis urbs fortitudinis eius pavor pauperum egestas eorum
16 Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
opus iusti ad vitam fructus impii ad peccatum
17 Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
via vitae custodienti disciplinam qui autem increpationes relinquit errat
18 Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
abscondunt odium labia mendacia qui profert contumeliam insipiens est
19 Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
in multiloquio peccatum non deerit qui autem moderatur labia sua prudentissimus est
20 Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
argentum electum lingua iusti cor impiorum pro nihilo
21 Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
labia iusti erudiunt plurimos qui autem indocti sunt in cordis egestate morientur
22 Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
benedictio Domini divites facit nec sociabitur ei adflictio
23 Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
quasi per risum stultus operatur scelus sapientia autem est viro prudentia
24 Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
quod timet impius veniet super eum desiderium suum iustis dabitur
25 Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
quasi tempestas transiens non erit impius iustus autem quasi fundamentum sempiternum
26 Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
sicut acetum dentibus et fumus oculis sic piger his qui miserunt eum
27 Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
timor Domini adponet dies et anni impiorum breviabuntur
28 Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
expectatio iustorum laetitia spes autem impiorum peribit
29 Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
fortitudo simplicis via Domini et pavor his qui operantur malum
30 Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
iustus in aeternum non commovebitur impii autem non habitabunt in terram
31 Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
os iusti parturiet sapientiam lingua pravorum peribit
32 Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.
labia iusti considerant placita et os impiorum perversa

< Mithali 10 >