< Mithali 10 >
1 Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
ソロモンの箴言 智慧ある子は父を欣ばす 愚なる子は母の憂なり
2 Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
不義の財は益なし されど正義は救ひて死を脱かれしむ
3 Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
ヱホバは義者の霊魂を餓ゑしめず 惡者にその欲するところを得ざらしむ
4 Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
手をものうくして動くものは貧くなり 勤めはたらく者の手は富を得
5 Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
夏のうちに斂むる者は智き子なり 収穫の時にねむる者は辱をきたす子なり
6 Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
義者の首には福祉きたり 惡者の口は強暴を掩ふ
7 Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
義者の名は讃られ 惡者の名は腐る
8 Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
心の智き者は誡命を受く されど口の頑愚なる者は滅さる
9 Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
直くあゆむ者はそのあゆむこと安し されどその途を曲ぐる者は知らるべし
10 Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
眼をもて眴せする者は憂をおこし 口の頑愚なる者は亡さる
11 Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
義者の口は生命の泉なり 惡者の口は強暴を掩ふ
12 Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
怨恨は爭端をおこし 愛はすべての愆を掩ふ
13 Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
哲者のくちびるには智慧あり 智慧なき者の背のためには鞭あり
14 Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
智慧ある者は知識をたくはふ 愚かなる者の口はいまにも滅亡をきたらす
15 Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
富者の資財はその堅き城なり 貧者のともしきはそのほろびなり
16 Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
義者が動作は生命にいたり 惡者の利得は罪にいたる
17 Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
敎をまもる者は生命の道にあり懲戒をすつる者はあやまりにおちいる
18 Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
怨をかくす者には虚偽のくちびるあり 誹謗をいだす者は愚かなる者なり
19 Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
言おほけれぼ罪なきことあたはず その口唇を禁むるものは智慧あり
20 Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
義者の舌は精銀のごとし 惡者の心は値すくなし
21 Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
義者の口唇はおほくの人をやしなひ 愚なる者は智慧なきに由て死ぬ
22 Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
ヱホバの祝福は人を富す 人の勞苦はこれに加ふるところなし
23 Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
愚かなる者は惡をなすを戯れごとのごとくす 智慧のさとかる人にとりても是のごとし
24 Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
惡者の怖るるところは自己にきたり 義者のねがふところはあたへらる
25 Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
狂風のすぐるとき惡者は無に歸せん 義者は窮なくたもつ基のごとし
26 Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
惰る者のこれを遣すものに於るは酢の歯に於るが如く煙の目に於るが如し
27 Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
ヱホバを畏るることは人の日を多くす されど惡者の年はちぢめらる
28 Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
義者の望は喜悦にいたり惡者の望は絶べし
29 Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
ヱホバの途は直者の城となり 惡を行ふものの滅亡となる
30 Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
義者は何時までも動かされず 惡者は地に住むことを得じ
31 Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
義者の口は智慧をいだすなり 虚偽の舌は抜るべし
32 Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.
義者のくちびるは喜ばるべきことをわきまへ 惡者の口はいつはりを語る