< Mithali 10 >

1 Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
Proverbi di Salomone. Un figliuol savio rallegra suo padre, ma un figliuolo stolto è il cordoglio di sua madre.
2 Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
I tesori d’empietà non giovano, ma la giustizia libera dalla morte.
3 Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
L’Eterno non permette che il giusto soffra la fame, ma respinge insoddisfatta l’avidità degli empi.
4 Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
Chi lavora con mano pigra impoverisce, ma la mano dei diligenti fa arricchire.
5 Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
Chi raccoglie nella estate è un figliuolo prudente, ma chi dorme durante la raccolta è un figliuolo che fa vergogna.
6 Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
Benedizioni vengono sul capo dei giusti, ma la violenza cuopre la bocca degli empi.
7 Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
La memoria del giusto e in benedizione, ma il nome degli empi marcisce.
8 Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
Il savio di cuore accetta i precetti, ma lo stolto di labbra va in precipizio.
9 Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
Chi cammina nella integrità cammina sicuro, ma chi va per vie tortuose sarà scoperto.
10 Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
Chi ammicca con l’occhio cagiona dolore, e lo stolto di labbra va in precipizio.
11 Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
La bocca del giusto è una fonte di vita, ma la bocca degli empi nasconde violenza.
12 Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
L’odio provoca liti, ma l’amore cuopre ogni fallo.
13 Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
Sulle labbra dell’uomo intelligente si trova la sapienza, ma il bastone è per il dosso di chi è privo di senno.
14 Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
I savi tengono in serbo la scienza, ma la bocca dello stolto e una rovina imminente.
15 Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
I beni del ricco sono la sua città forte; la rovina de’ poveri è la loro povertà.
16 Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
Il lavoro del giusto serve alla vita, le entrate dell’empio servono al peccato.
17 Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
Chi tien conto della correzione, segue il cammino della vita; ma chi non fa caso della riprensione si smarrisce.
18 Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
Chi dissimula l’odio ha labbra bugiarde, e chi spande la calunnia è uno stolto.
19 Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
Nella moltitudine delle parole non manca la colpa, ma chi frena le sue labbra è prudente.
20 Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
La lingua del giusto è argento eletto; il cuore degli empi val poco.
21 Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
Le labbra del giusto pascono molti, ma gli stolti muoiono per mancanza di senno.
22 Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
Quel che fa ricchi è la benedizione dell’Eterno e il tormento che uno si dà non le aggiunge nulla.
23 Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
Commettere un delitto, per lo stolto, è come uno spasso; tale è la sapienza per l’uomo accorto.
24 Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
All’empio succede quello che teme, ma ai giusti è concesso quel che desiderano.
25 Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
Come procella che passa, l’empio non è più, ma il giusto ha un fondamento eterno.
26 Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Come l’aceto ai denti e il fumo agli occhi, così è il pigro per chi lo manda.
27 Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
Il timor dell’Eterno accresce i giorni ma gli anni degli empi saranno accorciati.
28 Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
L’aspettazione dei giusti è letizia, ma la speranza degli empi perirà.
29 Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
La via dell’Eterno è una fortezza per l’uomo integro, ma una rovina per gli operatori d’iniquità.
30 Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
Il giusto non sarà mai smosso, ma gli empi non abiteranno la terra.
31 Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
La bocca del giusto sgorga sapienza, ma la lingua perversa sarà soppressa.
32 Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.
Le labbra del giusto conoscono ciò che è grato, ma la bocca degli empi e piena di perversità.

< Mithali 10 >