< Mithali 10 >

1 Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
L'enfant sage réjouit son père, mais l'enfant insensé est l'ennui de sa mère.
2 Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
Les trésors de méchanceté ne profiteront de rien; mais la justice garantira de la mort.
3 Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
L'Eternel n'affamera point l'âme du juste; mais la malice des méchants les pousse au loin.
4 Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
La main paresseuse fait devenir pauvre; mais la main des diligents enrichit.
5 Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
L'enfant prudent amasse en été; [mais] celui qui dort durant la moisson, est un enfant qui fait honte.
6 Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
Les bénédictions seront sur la tête du juste; mais la violence couvrira la bouche des méchants.
7 Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
La mémoire du juste sera en bénédiction; mais la réputation des méchants sera flétrie.
8 Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
Le sage de cœur recevra les commandements; mais le fou de lèvres tombera.
9 Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
Celui qui marche dans l'intégrité, marche en assurance; mais celui qui pervertit ses voies, sera connu.
10 Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
Celui qui fait signe de l'œil, donne de la peine; et le fou de lèvres sera renversé.
11 Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
La bouche du juste est une source de vie; mais l'extorsion couvrira la bouche des méchants.
12 Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
La haine excite les querelles; mais la charité couvre tous les forfaits.
13 Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
La sagesse se trouve sur les lèvres de l'homme intelligent; mais la verge est pour le dos de celui qui est dépourvu de sens.
14 Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
Les sages mettent en réserve la science; mais la bouche du fou [est] une ruine prochaine.
15 Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
Les biens du riche sont la ville de sa force; mais la pauvreté des misérables est leur ruine.
16 Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
L'œuvre du juste tend à la vie; mais le rapport du méchant tend au péché.
17 Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
Celui qui garde l'instruction, tient le chemin qui tend à la vie; mais celui qui néglige la correction, se fourvoie.
18 Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
Celui qui couvre la haine, use de fausses lèvres; et celui qui met en avant des choses diffamatoires, est fou.
19 Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
La multitude des paroles n'est pas exempte de péché; mais celui qui retient ses lèvres, est prudent.
20 Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
La langue du juste est un argent choisi; mais le cœur des méchants est bien peu de chose.
21 Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
Les lèvres du juste en instruisent plusieurs; mais les fous mourront faute de sens.
22 Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
La bénédiction de l'Eternel est celle qui enrichit, et [l'Eternel] n'y ajoute aucun travail.
23 Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
C'est comme un jeu au fou de faire quelque méchanceté; mais la sagesse est de l'homme intelligent.
24 Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
Ce que le méchant craint, lui arrivera; mais [Dieu] accordera aux justes ce qu'ils désirent.
25 Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
Comme le tourbillon passe, ainsi le méchant n'est plus; mais le juste est un fondement perpétuel.
26 Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Ce qu'est le vinaigre aux dents, et la fumée aux yeux; tel est le paresseux à ceux qui l'envoient.
27 Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
La crainte de l'Eternel accroît le nombre des jours; mais les ans des méchants seront retranchés.
28 Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
L'espérance des justes n'est que joie; mais l'attente des méchants périra.
29 Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
La voie de l'Eternel est la force de l'homme intègre; mais elle est la ruine des ouvriers d'iniquité.
30 Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
Le juste ne sera jamais ébranlé; mais les méchants n'habiteront point en la terre.
31 Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
La bouche du juste produira la sagesse; mais la langue hypocrite sera retranchée.
32 Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.
Les lèvres du juste connaissent ce qui est agréable; mais la bouche des méchants n'est que renversements.

< Mithali 10 >