< Wafilipi 1 >
1 Paulo na Timotheo, watumishi wa Kristo Yesu, Kwa wale walitengwa katika Kristo wanaoishi Filipi, pamoja na waangalizi na mashemasi.
Pavel in Timotej, hlapca Jezusa Kristusa, vsem svetim v Kristusu Jezusu bivajočim v Filipih, z vladikami in pomočniki.
2 Neema na iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
Milost vam in mir od Boga očeta našega in Gospoda Jezusa Kristusa!
3 Namshukuru Mungu wangu kila ninapowakumbuka ninyi nyote.
Zahvaljujem se Bogu svojemu, kader se vas spominjam.
4 Mara zote katika kila ombi langu kwa ajili yenu ninyi nyote, huwa na furahi ninapowaombea.
(Ko vedno v sleherni molitvi svoji molim za vas vse z veseljem),
5 Nina shukrani nyingi kwa sababu ya ushirika wenu katika injili tangu siku ya kwanza mpaka leo.
Da ste se udeleževali evangelja od prvega do današnjega dne;
6 Nina hakika kuwa yeye aliyeanzisha kazi njema ndani yenu ataendelea kuikamilisha mpaka siku ya Bwana Yesu Kristo.
Prepričan prav tega, da bode on, ki je začel v vas dobro delo, dokončal ga do dné Jezusa Kristusa;
7 Ni sawa kwangu kujisikia hivi juu yenu ninyi nyote kwa sababu nimewaweka moyoni wangu. Maana ninyi mmekuwa washirika wenza katika neema katika kifungo changu na katika utetezi na uthibitishaji wangu wa injili.
Kakor je meni spodobno misliti za vas vse, ker vas imam v srci, v sponah svojih in zagovarjanji in utrjevanji evangelja, ki ste vsi sodeležniki mi milosti.
8 Mungu ni shahidi wangu, jinsi nilivyo na shauku juu ya yenu nyote katika undani wa pendo la Kristo Yesu.
Kajti priča mi je Bog, kako hrepenim po vas vseh z osrčjem Jezusa Kristusa.
9 Na ninaomba kwamba: upendo wenu uongezeke zaidi na zaidi katika maarifa na ufahamu wote.
In tudi to molim, da naj ljubezen vaša še bolj in bolj raste v spoznanji in slehernem razumu;
10 Ninaomba kwa ajili ya hili ili muwe na uwezo wa kupima na kuchagua mambo yaliyo bora sana. Pia ninawaombea ili muwe safi pasipokuwa na hatia yoyote katika siku ya Kristo.
Da presojate, kar je imenitno, da bodete čisti in neizpotakljivi za dan Kristusov,
11 Na pia ili mjazwe na tunda la haki lipatikanalo katika Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa ya Mungu.
Napolnjeni sè sadom pravice po Jezusu Kristusu v slavo in hvalo Božjo.
12 Sasa ndugu zangu, nataka mjue kuwa, mambo yaliyotokea kwangu yameifanya injili iendelee sana.
Želim pa, da spoznate, bratje, da je stanje moje postalo bolj v uspeh evangelju,
13 Ndiyo maana vifungo vyangu katika Kristo, vimejulikana kwa walinzi wa ikulu yote na kwa kila mtu pia.
Tako da so spone moje očitne postale, da so v Kristusu v vsem šatorišči telesne straže in vsem drugim,
14 Na ndugu wengi katika Bwana, kwa sababu ya vifungo vyangu, wameshawishika na kuthubutu kulihubiri Neno pasipo hofu.
In da večina bratov v Gospodu zaupajoč mojim sponam upa se bolj brez strahu govoriti besedo.
15 Baadhi kweli hata humtangaza Kristo kwa fitina na ugomvi, na pia wengine kwa nia njema.
Nekateri tudi iz nevoščljivosti in prepirljivosti, nekateri pa tudi iz dobre volje oznanjajo Kristusa.
16 Wale wanaomtangaza Kristo kwa upendo wanajua kuwa nimewekwa hapa kwa ajili ya utetezi wa injili.
Oni, ki iz prepirljivosti, ne oznanjajo Kristusa iz čistega namena, češ da prinesó stisko sponam mojim;
17 Bali wengine wanamtangaza Kristo kwa ubinafsi na nia mbaya. Hudhani kuwa wanasababisha matatizo kwangu katika minyororo yangu.
Kateri pa iz ljubezni, vedóč, da sem pripravljen v zagovarjanje evangelja.
18 Kwa hiyo? Sijali, aidha njia ikiwa ni kwa hila au kwa kweli, Kristo anatangazwa, na katika hili ninafurahia! Ndiyo, nitafurahia.
Kaj pač? Vendar tako ali tako, bodi si s pretvezo, bodi si v resnici, oznanja se Kristus; in tega se veselim, dà, bodem se tudi veselil.
19 kwa kuwa ninajua ya kuwa hili litaleta kufunguliwa kwangu. Jambo hili litatokea kwa sababu ya maombi yenu na kwa msaada wa Roho wa Yesu Kristo.
Vem namreč, da mi bode to v blaginjo po prošnji vaši in pomoči duha Jezusa Kristusa,
20 Kulingana na matarajio yangu ya uhakika na kweli ni kwamba, sitaona aibu. Badala yake, kwa ujasiri wote, kama ambavyo siku zote na sasa, natarajia kuwa Kristo atainuliwa katika mwili wangu, ikiwa katika uzima au katika kifo.
Po pričakovanji in upanji mojem, da se v ničemur ne osramotim, temuč v vsej prostodušnosti, kakor vedno, bode se tudi sedaj Kristus poveličeval v mojem telesu, bodi si z življenjem, bodi si sè smrtjo.
21 Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo na kufa ni faida.
Kajti meni je življenje Kristus, in smrt dobiček.
22 Lakini, kama kuishi katika mwili huzaa tunda katika kazi yangu, kwa hiyo sijui ni lipi la kuchagua.
Ako pa življenje v mesu, to mi je dela sad, in kaj bodem izvolil, ne vem;
23 Maana ninasukumwa sana na mawazo haya mawili. Nina hamu ya kuuacha mwili na kuwa pamoja na Kristo, kitu ambacho ni cha thamani sana sana.
Kajti pritiska me oboje, želja me je ločiti se in biti s Kristusom, mnogo je namreč bolje;
24 Ingawa, kubaki katika mwili huu ni jambo la muhimu sana kwa ajili yenu.
Ostati pa v mesu potrebnejše za voljo vas.
25 Kwa kuwa nina uhakika juu ya hili, ninajua nitabaki na kuendelea kuwa pamoja nanyi nyote, kwa ajili ya maendeleo na furaha ya imani yenu.
In v tem zaupanji vem, da bodem ostal in z vami vsemi skupaj ostal v pospeh vaš in veselje v veri,
26 Na hii italeta furaha yenu kubwa katika Kristo Yesu, kwasababu yangu itaongezeka, kwa sababu ya uwepo wangu tena pamoja nanyi.
Da bode slava vaša preobila v Kristusu Jezusu v meni, zaradi povrnitve moje k vam.
27 Mnatakiwa kuishi maisha yenu katika mwenendo mzuri uipasayo injili ya Kristo. fanyeni hivyo ili nikija kuwaona au nisipokuja, nisikie kuwa mmesimama imara katika roho moja. natamani kusikia kuwa mna roho moja, mkiishindania imani ya injili kwa pamoja.
Samo védite se spodobno evangelju Kristusovemu, da bodem, bodi si, da pridem in vidim, bodi si v daljavi, slišal, kako je pri vas, da stojite trdno v enem duhu, eni duši, vkup boreč se za vero evangelja,
28 na msitishwe na kitu chochote kinachofanywa na maadui zenu. Hii kwao ni ishara ya uharibifu. Bali kwenu ni ishara ya wokovu kutoka kwa Mungu.
In da vas nikakor ne strašijo nasprotniki; kar je njim znamenje pogube, vam pa blaginje, in to od Boga;
29 kwa maana ninyi mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, bali na kuteswa pia katika Yeye.
Ker vam je bilo podeljeno za Kristusa, ne samo verovati vanj, nego tudi zanj trpeti;
30 kwa maana mna mgogoro uleule kama mliouona kwangu na mnasikia kwamba ninao hata sasa.
Ko imate isti boj, katerega ste videli v meni, in zdaj slišite v meni.