< Wafilipi 3 >

1 Hatimaye, ndugu zangu furahini katika Bwana. Sioni usumbufu kuwaandikia tena maneno yaleyale. Haya mambo yatawapa usalama.
Finally, my brethren, rejoice in the Lord. To write the same things to you is to me indeed not burdensome; but for you it is safe.
2 Jihadharini na mbwa. Jihadharini na watenda kazi wabaya. Jihadharini na wale wajikatao miili yao.
Beware of the dogs, beware of the evil workers, beware of the concision.
3 Kwa kuwa sisi nndiyo tohara. Sisi ndiyo huwa tumwabudu Mungu kwa msaada wa Roho. Tujivuniao katika Kristo Yesu, na ambao hatuna ujasiri katika mwili.
For we are the circumcision, who worship God in spirit, and rejoice in Christ Jesus, and have no confidence in the flesh;
4 Hata hivyo, kama kungekuwa na mtu wa kuutumainia mwili huu, mimi ningeweza kufanya hivyo zaidi.
though, indeed, I have a ground of confidence in the flesh. If any other thinks he has a ground of confidence in the flesh, I more;
5 Kwani nilitahiriwa siku ya nane, nilizaliwa katika kabila la Waisraeli. Ni wa kabila la Benjamini. Ni Mwebrania wa waebrani. Katika kuitimiza haki ya sheria ya Musa, nilikuwa, Farisayo.
circumcised the eighth day, of the race of Israel, of the tribe of Benjamin, a Hebrew of the Hebrews; as it respects law, a Pharisee;
6 Kwa juhudi zangu nililitesa Kanisa. Kwa tuitii haki ya sheria, sikuwa na lawama kisheria.
as it respects zeal, persecuting the church; as it respects righteousness which is by law, blameless.
7 Lakini katika mambo yote niliyoyaona kuwa ya faida kwangu mimi, niliyahesabu kama takataka kwa sababu ya kumfahamu Kristo.
But the things which were gain to me, these I counted loss for Christ.
8 Kwa kweli, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kutokana ubora wa kumjua wa Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimeaacha mambo yote, nayahesabu kama takataka ili nimpate Kristo
Yes, verily, I also count all things to be loss, for the excellence of the knowledge of Christ Jesus my Lord, on account of whom I have suffered the loss of all things, and do count them to be refuse, that I may gain Christ,
9 na nionekane ndani yake. Sina haki yangu binafisi kutoka katika sheria, bali ninayo haki ile ipatikanayo kwa imani katika Kristo, itokayo kwa Mungu, yenye msingi katika imani.
and be found in him, not having my own righteousness which was by law, but the righteousness which is by faith in Christ, the righteousness which is of God by faith,
10 Sasa nataka kumfahamu yeye na nguvu ya ufufuo wake na ushirika wa mateso yake. Nataka kubadilishwa na Kristo katika mfano wa kifo chake,
that I may know him, and the power of his resurrection, and the fellowship of his sufferings, by conforming myself to his death,
11 angalau niweze kuwa na matumaini katika ufufuo wa wafu.
if, by any means, I may attain to the resurrection from the dead.
12 Siyo kweli kwamba tayari nimeishayapata mambo hayo, au kwamba nimekuwa mkamilifu katika hayo. Bali najitahidi ili niweze kupata kile kupata kile nilichopatikana na Kristo Yesu.
Not that I have already attained, or have already reached the goal; but I am pressing forward, that I may lay hold on that for which I was laid hold on by Christ Jesus.
13 Ndugu zangu, sidhani kwamba nimekwisha kupata mambo haya. Bali nafanya jambo moja: nasahau ya nyuma nayatazamia ya mbele.
Brethren, I do not conclude that I have already laid hold:
14 Najitahidi kufikia lengo kusudi ili nipate tuzo ya juu ya wito wa Mungu katika Kristo Yesu.
but one thing I do; forgetting the things which are behind, and reaching forward to those which are before, I press toward the goal, for the prize of the high calling of God in Christ Jesus.
15 Sote tulio ukulia wokovu, tunapaswa kuwaza namna hii. Na ikiwa mwingine atafikiri kwa namna iliyotofauti kuhusu jambo lo lote, Mungu pia atalifunuao hiilo kwenu.
Let us, therefore, as many as are fully enlightened, be of this mind: and if you are of another mind with respect to any thing, God will reveal even this to you.
16 Hata hivyo, hatua ifikia na tuenende katika mtindo huo.
But as far as we have attained, let us walk by the same rule, let us have the same mind.
17 Ndugu zangu, niigeni mimi. Waangalieni kwa makini wale wanaoenenda kwa mfano ulio wa jinsi yetu.
Be imitators of me, brethren, and observe those who thus walk as you have us for an example.
18 Wengi wanaoishi niwale ambao mara nyingi nimewaambieni, na sasa nawaambia kwa machozi -wengi wanaishi kama maadui wa msalaba wa Kristo.
For many walk, of whom I often said to you, and now say even weeping, that they are enemies of the cross of the Christ,
19 Mwisho wao ni uharibifu. Kwa kuwa Mungu wao ni tumbo, na kiburi chao kiko katika aibu yao. Wanafikiria mambo ya kidunia.
whose end is destruction, whose god is their appetite, and whose glory is in their shame, who mind earthly things.
20 Bali uraia wetu uko mbinguni, ambako tunamtarajia mwokozi wetu Yesu Kristo.
But our citizenship is in heaven, whence also we look for the Savior, the Lord Jesus Christ,
21 Atabadilisha miili yetu dhaifu kuwa kama mwili wake wa utukufu; kwa uweza ule ule unaomwezesha kuvidhibiti vitu vyote.
who will transform our humbled body, and make it like his glorious body, according to that power by which he is able to subdue all things to himself.

< Wafilipi 3 >