< Filemoni 1 >

1 Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na ndugu Timotheo kwa Filemoni, mpendwa rafiki yetu na mtenda kazi pamoja nasi,
Pablo, prisionero de Jesucristo, y Timoteo nuestro hermano, a Filemón, nuestro querido ayudante en la fe,
2 na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipas askari mwenzetu, na kwa kanisa lile linalokutana nyumbani kwako.
Y a Apia, nuestra hermana, y a Arquipo, nuestro hermano en el ejército de Dios, y a la iglesia en tu casa.
3 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Gracia y paz a ustedes de parte de Dios nuestro Padre y del Señor Jesucristo.
4 Wakati wote namshukuru Mungu. Ninakutaja katika maombi yangu.
Alabaré a Dios en todo tiempo y oraré por ti,
5 Nimesikia upendo na imani uliyonayo katika Bwana Yesu na kwa ajili ya waumini wote.
Escuchando el amor y la fe que tienes para el Señor Jesús y para todos los santos;
6 Ninaomba kwamba ushirika wa imani yenu iwe na ufanisi katika ujuzi wa kila jambo jema lililoko kati yetu katika Kristo.
Para que la fe que tienes en común con ellos obre con poder, en el conocimiento de todo lo bueno que hay en ti, para Cristo.
7 Kwa kuwa nimekuwa na furaha na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa sababu mioyo ya waumini imekuwa ikitulizwa nawe, ndugu.
Porque tuve gran gozo y consuelo en tu amor, porque los corazones de los santos se han fortalecido por medio de ti, hermano.
8 Kwa hiyo, ingawa nina ujasiri wote katika Kristo kukuamuru wewe kufanya kile unachoweza kufanya,
Y así, aunque podría, en nombre de Cristo, darte órdenes de hacer lo correcto,
9 lakini kwa sababu ya upendo, badala yake nakusihi - mimi, Paulo niliye mzee, na sasa ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu.
Aún así, por amor, en lugar de una orden, te hago una petición, yo, Pablo, un anciano y ahora un prisionero de Cristo Jesús.
10 Ninakusihi kuhusu mwanangu Onesmo, niliyemzaa katika vifungo vyangu.
Mi petición es para mi hijo Onésimo, el hijo de mis cadenas,
11 Kwa kuwa mwanzoni hakukufaa, lakini sasa anakufaa wewe na mimi.
Que en el pasado no te servía de nada, pero que ahora te beneficia a ti y a mí:
12 Nimemtuma- yeye ambaye ni wa moyo wangu hasa - kurudi kwako.
A quien he enviado a ti, tu, pues, recíbele como a mi mismo:
13 Nataraji angeendelea kubaki pamoja nami, ili anitumikie badala yako, wakati niwako kifungoni kwa ajili ya injili.
Aunque mi deseo era mantenerlo conmigo, ser mi siervo en las cadenas de las buenas nuevas, en tu lugar:
14 Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ruhusa yako. Nilifanya hivi ili kwamba jambo lolote zuri lisifanyike kwa sababu nilikulazimisha, bali kwa sababu ulipenda mwenyewe kulitenda.
Pero sin tu aprobación no haría nada; para que tus buenas obras no sean forzadas, sino hechas libremente desde tu corazón.
15 Labda ni sababu alitengwa nawe kwa muda, ilikuwa hivyo ili uwe pamoja naye milele. (aiōnios g166)
Porque es posible que por esta razón él se separó de ti por un tiempo, para que puedas recibirlo para siempre; (aiōnios g166)
16 Ili kwamba asiwe tena mtumwa, bali bora zaidi ya mtumwa, kama ndugu mpendwa, hasa kwangu, na zaidi sana kwako, katika mwili na katika Bwana.
Ya no como siervo, sino más que como siervo, como hermano, muy querido para mí especialmente, pero mucho más para ti, tanto en la carne como en el Señor.
17 Na hivyo kama wanichukulia mimi mshirika, mpokee kama ambavyo ungenipokea mimi.
Si luego me llevas a ser tu amigo y hermano, acéptalo como a mí mismo.
18 Lakini kama amekukosea jambo lolote, au unamdai kitu chochote, kidai hicho kutoka kwangu.
Si él te ha hecho algo malo o está en deuda contigo por algo, póngalo en mi cuenta.
19 Mimi Paulo, ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe: mimi nitakulipa. Sisemi kwako kwamba nakudai maisha yako hasa.
Yo, Pablo, escribiéndolo yo mismo, te digo: te pagaré; y no te digo que estás en deuda conmigo, por tu propia vida.
20 Naam ndugu, acha nipate furaha ya Bwana toka kwako: uburudishe moyo wangu katika Kristo.
Así que hermano, como cristiano se generoso conmigo en él Señor: consuela mi corazón en Cristo.
21 Nikiwa na imani kuhusu utii wako, nakuandikia nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya vile ninavyokuomba.
Estoy seguro de que harás mi deseo, te escribo, sabiendo que harás incluso más de lo que digo.
22 Wakati huo huo andaa chumba cha wageni kwa ajili yangu, kwa kuwa ninatumaini kupitia maombi yako nitakutembelea hivi karibuni.
Y prepárame una habitación; porque espero que a través de sus oraciones pueda venir a ustedes.
23 Epafra, mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu anakusalimu,
Epafras, mi hermano, prisionero en Cristo Jesús, te envía saludos;
24 na kama afanyavyo Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi pamoja nami.
Y también Marcos, Aristarco, Demas y Lucas, mis hermanos trabajadores.
25 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako. Amina.
La gracia de nuestro Señor Jesucristo sea derramada sobre ustedes. Amen.

< Filemoni 1 >