< Filemoni 1 >

1 Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na ndugu Timotheo kwa Filemoni, mpendwa rafiki yetu na mtenda kazi pamoja nasi,
Pablo, prisionero de Cristo Jesús, y el hermano Timoteo, al querido Filemón, colaborador nuestro,
2 na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipas askari mwenzetu, na kwa kanisa lile linalokutana nyumbani kwako.
y a Apia, la hermana, y a Arquipo nuestro compañero de armas, y a la Iglesia que está en tu casa:
3 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
gracia a vosotros y paz, de parte de Dios Nuestro Padre, y del Señor Jesucristo.
4 Wakati wote namshukuru Mungu. Ninakutaja katika maombi yangu.
Doy gracias a mi Dios, haciendo sin cesar memoria de ti en mis oraciones,
5 Nimesikia upendo na imani uliyonayo katika Bwana Yesu na kwa ajili ya waumini wote.
porque oigo hablar de tu caridad y de la fe que tienes para el Señor Jesús y para con todos los santos;
6 Ninaomba kwamba ushirika wa imani yenu iwe na ufanisi katika ujuzi wa kila jambo jema lililoko kati yetu katika Kristo.
a fin de que la participación de tu fe sea eficaz para que se conozca todo el bien que hay en vosotros en relación con Cristo.
7 Kwa kuwa nimekuwa na furaha na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa sababu mioyo ya waumini imekuwa ikitulizwa nawe, ndugu.
Tuve mucho gozo y consuelo con motivo de tu caridad, por cuanto los corazones de los santos han hallado alivio por ti, hermano.
8 Kwa hiyo, ingawa nina ujasiri wote katika Kristo kukuamuru wewe kufanya kile unachoweza kufanya,
Por lo cual, aunque tengo toda libertad en Cristo para mandarte lo que conviene,
9 lakini kwa sababu ya upendo, badala yake nakusihi - mimi, Paulo niliye mzee, na sasa ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu.
prefiero, sin embargo, rogarte a título de amor, siendo como soy, Pablo, el anciano y ahora además prisionero de Cristo Jesús.
10 Ninakusihi kuhusu mwanangu Onesmo, niliyemzaa katika vifungo vyangu.
Te ruego, pues, por mi hijo Onésimo, a quien he engendrado entre cadenas,
11 Kwa kuwa mwanzoni hakukufaa, lakini sasa anakufaa wewe na mimi.
el cual en un tiempo te fue inútil, mas ahora es muy útil para ti y para mí.
12 Nimemtuma- yeye ambaye ni wa moyo wangu hasa - kurudi kwako.
Te lo devuelvo; tú, empero, recíbelo a él como a mi propio corazón.
13 Nataraji angeendelea kubaki pamoja nami, ili anitumikie badala yako, wakati niwako kifungoni kwa ajili ya injili.
Quisiera retenerlo junto a mí, para que en tu nombre me sirviese en las cadenas por el Evangelio;
14 Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ruhusa yako. Nilifanya hivi ili kwamba jambo lolote zuri lisifanyike kwa sababu nilikulazimisha, bali kwa sababu ulipenda mwenyewe kulitenda.
pero sin consultarte no quise hacer nada, para que tu beneficio no fuese como forzado, sino voluntario.
15 Labda ni sababu alitengwa nawe kwa muda, ilikuwa hivyo ili uwe pamoja naye milele. (aiōnios g166)
Quizás por esto él se ha apartado por un tiempo, a fin de que lo tengas para siempre, (aiōnios g166)
16 Ili kwamba asiwe tena mtumwa, bali bora zaidi ya mtumwa, kama ndugu mpendwa, hasa kwangu, na zaidi sana kwako, katika mwili na katika Bwana.
no ya como siervo, sino más que siervo como hermano amado, amado para mí en particular, pero ¡cuánto más para ti, no solo en la carne sino en el Señor!
17 Na hivyo kama wanichukulia mimi mshirika, mpokee kama ambavyo ungenipokea mimi.
Si pues me tienes a mí por compañero, acógelo como a mí mismo.
18 Lakini kama amekukosea jambo lolote, au unamdai kitu chochote, kidai hicho kutoka kwangu.
Si en algo te ha perjudicado o te debe, ponlo a mi cuenta.
19 Mimi Paulo, ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe: mimi nitakulipa. Sisemi kwako kwamba nakudai maisha yako hasa.
Yo Pablo lo escribo con mi propia mano; yo lo pagaré, por no decirte que tú, tú mismo, te me debes.
20 Naam ndugu, acha nipate furaha ya Bwana toka kwako: uburudishe moyo wangu katika Kristo.
Sí, hermano, obtenga yo de ti gozo en el Señor, alivia mi corazón en Cristo.
21 Nikiwa na imani kuhusu utii wako, nakuandikia nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya vile ninavyokuomba.
Te escribo, confiando en tu obediencia, sabiendo que harás todavía más de lo que digo.
22 Wakati huo huo andaa chumba cha wageni kwa ajili yangu, kwa kuwa ninatumaini kupitia maombi yako nitakutembelea hivi karibuni.
Y al mismo tiempo prepara hospedaje para mí; pues espero que por vuestras oraciones os he de ser restituido.
23 Epafra, mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu anakusalimu,
Te saluda Epafras, mi compañero de cautiverio, en Cristo Jesús,
24 na kama afanyavyo Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi pamoja nami.
y Marcos, Aristarco, Demas y Lucas, mis colaboradores.
25 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako. Amina.
La gracia del Señor Jesucristo sea con vuestro espíritu. Amén.

< Filemoni 1 >