< Filemoni 1 >
1 Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na ndugu Timotheo kwa Filemoni, mpendwa rafiki yetu na mtenda kazi pamoja nasi,
Mi Bulus, vana inyang anyimo a Yessu nan Timoti uhenu uru uhana Ufilimon uhenu iriba iru, u roni ukatuma.
2 na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipas askari mwenzetu, na kwa kanisa lile linalokutana nyumbani kwako.
Uhana Aufiya ku henu kuru, nan unu tarsa Asere anyimo akura.
3 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Imumu i ruma iriba ishew ahira Asere nan i vana me Yesu i cukuno anyimo ashi.
4 Wakati wote namshukuru Mungu. Ninakutaja katika maombi yangu.
Ma guna Asere ankwoi barki shi anyimo abi ringara bum.
5 Nimesikia upendo na imani uliyonayo katika Bwana Yesu na kwa ajili ya waumini wote.
Barki ukunnna uhem ushi me nan unu ahira Asere nan aka tuma kameme.
6 Ninaomba kwamba ushirika wa imani yenu iwe na ufanisi katika ujuzi wa kila jambo jema lililoko kati yetu katika Kristo.
Inzin in biringara barkin u inko iriba ishi me nan umuta ace ashi me, i cukuno imumu ibezi ubari nan ure aje utize tiriri sa tizi tiru, barki Asere.
7 Kwa kuwa nimekuwa na furaha na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa sababu mioyo ya waumini imekuwa ikitulizwa nawe, ndugu.
Ma wuna iriba irum, iriba im ya totto barki uhenu umeme, mu riba ma hana Asere ma cukuno was barki hu.
8 Kwa hiyo, ingawa nina ujasiri wote katika Kristo kukuamuru wewe kufanya kile unachoweza kufanya,
Barki ani me, ca in gu barki Yesu, in zin in nikara in gun hu uwuzi vat imum be sa izi ihuma.
9 lakini kwa sababu ya upendo, badala yake nakusihi - mimi, Paulo niliye mzee, na sasa ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu.
Vat anime barki uhem, iteki in nnoki inmyira, mi Bulus ucokoro ana me be vana inyang barki Yesu.
10 Ninakusihi kuhusu mwanangu Onesmo, niliyemzaa katika vifungo vyangu.
In zini u igizo ushi abanga avana um Unisimas desa mazi mazi aco ameme uganiya ma raa anyimo inya.
11 Kwa kuwa mwanzoni hakukufaa, lakini sasa anakufaa wewe na mimi.
Uganiya me mazi imum ba ahira aweme ana me mazi imum ahira aru mi nan hu.
12 Nimemtuma- yeye ambaye ni wa moyo wangu hasa - kurudi kwako.
Mi monno ma tuburko me ahira aweme kasi nigoro ni iriba im.
13 Nataraji angeendelea kubaki pamoja nami, ili anitumikie badala yako, wakati niwako kifungoni kwa ajili ya injili.
Mazin uguna in inta me ahira am, ma wuzim katuma anyo aweme, uganiya sa ma raa anyimo inyan.
14 Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ruhusa yako. Nilifanya hivi ili kwamba jambo lolote zuri lisifanyike kwa sababu nilikulazimisha, bali kwa sababu ulipenda mwenyewe kulitenda.
Ani me in da nyara in wuzi iri mum sarki uhem uwe me ba, kati imum be sa u wuza i cukuno dake unu hem uweme ba.
15 Labda ni sababu alitengwa nawe kwa muda, ilikuwa hivyo ili uwe pamoja naye milele. (aiōnios )
Nani ine ini ya wuna ya harzina cingili, barki ikuri i gurna sarki ukuru harzina. (aiōnios )
16 Ili kwamba asiwe tena mtumwa, bali bora zaidi ya mtumwa, kama ndugu mpendwa, hasa kwangu, na zaidi sana kwako, katika mwili na katika Bwana.
Da kasi urerenba, ma aka ahira u rere, ma cukuno imumu wunairiba, ahira am nan a hira awe ahira atuma kani pum nan ka Asere.
17 Na hivyo kama wanichukulia mimi mshirika, mpokee kama ambavyo ungenipokea mimi.
Barki ani me ingi wa zikam uroni utanu kaba me kasi mime.
18 Lakini kama amekukosea jambo lolote, au unamdai kitu chochote, kidai hicho kutoka kwangu.
Ingi wa wuna imum i cara iriba, nani u tarsa me ire imum, kurzo ini ani ce num.
19 Mimi Paulo, ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe: mimi nitakulipa. Sisemi kwako kwamba nakudai maisha yako hasa.
Mi Bulus, mi mani ma nyertike in tari tum, indi kurzo we ni, katti u iri imum me sa ma wuza ani ce ni weme.
20 Naam ndugu, acha nipate furaha ya Bwana toka kwako: uburudishe moyo wangu katika Kristo.
U henu um, hem in kem iri mum sa inda perkem ba ahira aweme barki Asere, ca in kem imum be sa udi natim iriba barki Yesu.
21 Nikiwa na imani kuhusu utii wako, nakuandikia nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya vile ninavyokuomba.
Ma hem imumum be sa uwuzam, ine ini ya wunam ma nyertike, barki in rusa udi wuzi i aki imum be sa ma buka.
22 Wakati huo huo andaa chumba cha wageni kwa ajili yangu, kwa kuwa ninatumaini kupitia maombi yako nitakutembelea hivi karibuni.
A'ani me barkam ahira utotto, in inso iriba ahem in mi u aye ahira ashi me barki biringara bishi me.
23 Epafra, mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu anakusalimu,
Abafaras, uroni um sa atirin duru nan me barki Yesu, ma iso shi.
24 na kama afanyavyo Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi pamoja nami.
Ane ani Markus, Aristarkus, Dimas, nan Luka aroni aka tuma kam wa isoshi.
25 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako. Amina.
Ca mu riba mu shi me mu cukuno lau anyimo niza ni Yesu. Ni cukuno ani me.