< Filemoni 1 >

1 Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na ndugu Timotheo kwa Filemoni, mpendwa rafiki yetu na mtenda kazi pamoja nasi,
Paul, a prisoner of Messiah Jesus, and Timothy our brother, to Philemon, our beloved fellow worker,
2 na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipas askari mwenzetu, na kwa kanisa lile linalokutana nyumbani kwako.
and to Apphia our sister, to Archippus, our fellow soldier, and to the church in your house:
3 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus (the) Messiah.
4 Wakati wote namshukuru Mungu. Ninakutaja katika maombi yangu.
I thank my God always, making mention of you in my prayers,
5 Nimesikia upendo na imani uliyonayo katika Bwana Yesu na kwa ajili ya waumini wote.
hearing of your love, and of the faith which you have toward the Lord Jesus, and toward all the saints;
6 Ninaomba kwamba ushirika wa imani yenu iwe na ufanisi katika ujuzi wa kila jambo jema lililoko kati yetu katika Kristo.
that the fellowship of your faith may become effective, in the knowledge of every good thing which is in you in Messiah.
7 Kwa kuwa nimekuwa na furaha na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa sababu mioyo ya waumini imekuwa ikitulizwa nawe, ndugu.
For I have much joy and comfort in your love, because the hearts of the saints have been refreshed through you, brother.
8 Kwa hiyo, ingawa nina ujasiri wote katika Kristo kukuamuru wewe kufanya kile unachoweza kufanya,
Therefore, though I have all boldness in Messiah to command you that which is appropriate,
9 lakini kwa sababu ya upendo, badala yake nakusihi - mimi, Paulo niliye mzee, na sasa ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu.
yet on the basis of love I rather appeal, being such a one as Paul, the aged, but also a prisoner of Messiah Jesus.
10 Ninakusihi kuhusu mwanangu Onesmo, niliyemzaa katika vifungo vyangu.
I appeal to you for my child, whom I have become the father of in my chains, Onesimus,
11 Kwa kuwa mwanzoni hakukufaa, lakini sasa anakufaa wewe na mimi.
who once was useless to you, but now is useful to you and to me.
12 Nimemtuma- yeye ambaye ni wa moyo wangu hasa - kurudi kwako.
I am sending back to you, him who is my very heart,
13 Nataraji angeendelea kubaki pamoja nami, ili anitumikie badala yako, wakati niwako kifungoni kwa ajili ya injili.
whom I desired to keep with me, that on your behalf he might serve me in my chains for the gospel.
14 Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ruhusa yako. Nilifanya hivi ili kwamba jambo lolote zuri lisifanyike kwa sababu nilikulazimisha, bali kwa sababu ulipenda mwenyewe kulitenda.
But I was willing to do nothing without your consent, that your goodness would not be as of necessity, but of free will.
15 Labda ni sababu alitengwa nawe kwa muda, ilikuwa hivyo ili uwe pamoja naye milele. (aiōnios g166)
For perhaps he was therefore separated from you for a while, that you would have him forever, (aiōnios g166)
16 Ili kwamba asiwe tena mtumwa, bali bora zaidi ya mtumwa, kama ndugu mpendwa, hasa kwangu, na zaidi sana kwako, katika mwili na katika Bwana.
no longer as a slave, but more than a slave, a beloved brother, especially to me, but how much rather to you, both in the flesh and in the Lord.
17 Na hivyo kama wanichukulia mimi mshirika, mpokee kama ambavyo ungenipokea mimi.
If then you count me a partner, receive him as you would receive me.
18 Lakini kama amekukosea jambo lolote, au unamdai kitu chochote, kidai hicho kutoka kwangu.
But if he has wronged you at all, or owes you anything, put that to my account.
19 Mimi Paulo, ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe: mimi nitakulipa. Sisemi kwako kwamba nakudai maisha yako hasa.
I, Paul, write this with my own hand: I will repay it (not to mention to you that you owe to me even your own self besides).
20 Naam ndugu, acha nipate furaha ya Bwana toka kwako: uburudishe moyo wangu katika Kristo.
Yes, brother, let me have joy from you in the Lord. Refresh my heart in Messiah.
21 Nikiwa na imani kuhusu utii wako, nakuandikia nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya vile ninavyokuomba.
Having confidence in your obedience, I write to you, knowing that you will do even beyond what I say.
22 Wakati huo huo andaa chumba cha wageni kwa ajili yangu, kwa kuwa ninatumaini kupitia maombi yako nitakutembelea hivi karibuni.
Also, prepare a guest room for me, for I hope that through your prayers I will be restored to you.
23 Epafra, mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu anakusalimu,
Epaphras, my fellow prisoner in Messiah Jesus, greets you,
24 na kama afanyavyo Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi pamoja nami.
as do Mark, Aristarchus, Demas, and Luke, my fellow workers.
25 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako. Amina.
The grace of the Lord Jesus (the) Messiah be with your spirit.

< Filemoni 1 >