< Obadia 1 >

1 Maono ya Obadia. Bwana MUNGU asema hivi juu ya Edomu Tumesikia habari kutoka kwa Bwana, na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, akisema, Inukeni! Tuinuke dhidi yake kwa vita!”
The vision of Obadiah. This is what the Lord has said about Edom: We have had word from the Lord, and a representative has been sent among the nations, saying, Up! and let us make war against her.
2 Tazama, nitawafanya wadogo kati ya mataifa, mutadharauliwa sana.
See, I have made you small among the nations: you are much looked down on.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya wewe, wewe ambaye unishi katika makaburi ya miamba, katika nyumba yako ya juu; asemaye moyoni mwako, 'Ni nani atakayenishusha mimi chini?'
You have been tricked by the pride of your heart, O you whose living-place is in the cracks of the rock, whose house is high up; who has said in his heart, Who will make me come down to earth?
4 Ingawa unasimama juu kama tai na ingawa kiota chako huwekwa kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko, asema Yahweh.
Though you go up on high like an eagle, though your house is placed among the stars, I will make you come down from there, says the Lord.
5 Kama wezi walikuja kwako, ikiwa wanyang'anyi wangekujilia usiku (jinsi ungekatilwa mbali!), Wasingeweza kuiba vya kuwatosha? Ikiwa wakusanya zabibu wangekujilia, wasingeacha mavuno?
If thieves came, attacking you by night, (how are you cut off!) would they not go on taking till they had enough? if men came cutting your grapes would they take them all?
6 Jinsi Esau amekwisha kupigwa, na hazina zake zilizofichwa zimewekwa nje!
How are the things of Esau searched out! how are his secret stores looked for!
7 Watu wote wa ushirikiano wako watakupeleka katika njiani ya hadi mpakani. Watu waliokuwa na amani pamoja nawe wamekudanganya, na kukushinda. Wale wanaokula mkate wako wameweka mtego chini yako. Hakuna uelewa ndani yake.
All the men who were united with you have been false to you, driving you out to the edge of the land: the men who were at peace with you have overcome you; they have taken their heritage in your place.
8 Je! Sikuweza siku hiyo, asema Bwana, kuwaangamiza watu wenye hekima kutoka Edomu na kuelewa kutoka mlima wa Esau?
Will I not, in that day, says the Lord, take away the wise men out of Edom, and wisdom out of the mountain of Esau?
9 Mashujaa wako watafadhaika, Temani, ili kila mtu akatiliwe mbali kutoka mlima wa Esau kwa kuuawa.
And your men of war, O Teman, will be overcome with fear, so that every one of them may be cut off from the mountain of Esau.
10 Kwa sababu ya ukatili uliofanywa kwa ndugu yako Yakobo, utafunikwa na aibu, nawe utakatiliwa mbali milele.
Because you were the cause of violent death and because of your cruel behaviour to your brother Jacob, you will be covered with shame and will be cut off for ever.
11 Siku ile ulikuwa umesimama, siku wageni walichukua mali zake, na waliokuwa wageni katika malango yake, na kupiga kura kwa Yerusalemu, wewe ulikuwa kama mmoja wao.
Because you were there watching when men from other lands took away his goods, and strange men came into his doors, and put the fate of Jerusalem to the decision of chance; you were like one of them.
12 Lakini usifurahi siku ya ndugu yako, siku ya msiba wake, wala usifurahi juu ya watu wa Yuda siku ya uharibifu wao; msijisifu siku ya dhiki yao.
Do not see with pleasure your brother's evil day, the day of his fate, and do not be glad over the children of Judah on the day of their destruction, or make wide your mouth on the day of trouble.
13 Usiingie mlango wa watu wangu siku ya msiba wao; usifurahi juu ya taabu yao siku ya msiba wao, wala msipotee utajiri wao siku ya uharibifu wao.
Do not go into the doors of my people on the day of their downfall; do not be looking on their trouble with pleasure on the day of their downfall, or put your hands on their goods on the day of their downfall.
14 Usisimama kwenye njia panda, ili kuwakatilia mbali wakimbizi wake na usiwatoe waathirika wake katika siku ya dhiki.
And do not take your place at the cross-roads, cutting off those of his people who get away; and do not give up to their haters those who are still there in the day of trouble.
15 Kwa maana siku ya Bwana iko karibu na mataifa yote. Kama ulivyofanya, itafanyika kwako; matendo yako yatarudi juu ya kichwa chako mwenyewe.
For the day of the Lord is coming quickly on all nations: as you have done it will be done to you; the reward of your acts will come on your head.
16 Kwa vile mlivyokunywa katika mlima wangu mtakatifu, ndivyo mataifa yote yatakavyo kunywa daima. Watakunywa na kumeza na itakuwa kana kwamba hawakuwepo kabisa.
For as you have been drinking on my holy mountain, so will all the nations go on drinking without end; they will go on drinking and the wine will go down their throats, and they will be as if they had never been.
17 Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwa na wale waliookoka na watakuwa watakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki miliki zao.
But in Mount Zion some will be kept safe, and it will be holy; and the children of Jacob will take their heritage.
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yusufu ni mwali wa moto, na nyumba ya Esau itakuwa mabua makavu, nao watawaunguza, na kuwateketeza. Hakutakuwa na waathirika kwa nyumba ya Esau, kwa kuwa Bwana amesema.
And the children of Jacob will be a fire and those of Joseph a flame, and the children of Esau dry stems of grass, burned up by them till all is gone: and there will be no people living in Esau; for the Lord has said it.
19 Wote kutoka Negebu watamiliki mlima wa Esau na wale wa Shepela watamiliki nchi ya Wafilisti. Wao wataimiliki nchi ya Efraimu na nchi ya Samaria; na Benyamini atamiliki Gileadi.
And they will take the South, and the lowland, and the country of Ephraim, and Gilead, as their heritage.
20 Wahamiaji wa jeshi hili la watu wa Israeli watamiliki ardhi ya Kanaani mpaka Sarepta. Wahamiaji wa Yerusalemu, waliopo Sefaradi, wataimiliki miji ya Negebu.
And those of the children of Israel who were the first to be taken away as prisoners, will have their heritage among the Canaanites as far as Zarephath; and those who were taken away from Jerusalem, who are in Sepharad, will have the towns of the South.
21 Waokoaji watakwenda hadi juu ya Mlima Sayuni kutawala nchi ya vilima ya Esau, na ufalme utakuwa wa Bwana.
And those who have been kept safe will come up from Mount Zion to be judges of the mountain of Esau; and the kingdom will be the Lord's.

< Obadia 1 >